Jumatano, 6 Juni 2018

MAMIA WAJITOKEZA KUWAAGA MARIA NA CONSOLATA IRINGA

Posted by Esta Malibiche on JUNE 6,2018 IN NEWS


Jeneza lillobeba miili ya Maria na Consolata


 
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako akitoa heshima ya mwisho mbela ya jeneza lenye miili ya Maria na Consolata


Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako akisaini kitabu cha maombolezo
Naibu waziri ofisi ya waziri mkuu anaeshughulikia wenye ulemavu Stela Ikupa akisaini kitabu cha maombolezoa
Rais wa baraza la maaskofu katoliki Tanazania ambae pia ni Askofu wa jimbo  katoliki la Iringa Tarcisius Ngalalekumtwa akisaini kitabu cha maombolezo
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Albert Chalamila  akisaini kitabu cha maombolezo
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Christopher Magala  akisaini kitabu cha maombolezo
 Meya wa Manispaa ya Iringa,ambae ni Diwani wa kata ya Isakalilo  kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Alex Kimbe
Mbunge wa jimbo la Kalenga kupitia chama cha Mapinduzi CCM Goedfrey Mgimwa akisaini kitabu cha maombolezo
 Mwenyekiti wa jumuiya vijana wa umoja wa ccm Mkoa wa Iringa  UVCCM Kenani Kihongosi akisaini kitabu cha maombolezo.
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha Mapinduzi CCM Ritha Kabati akisaini kitabu cha maombolezo.
  Mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake ccm Mkoa wa Iringa Nicoli[UWT]akisaini kitabu cha maombolezo



 Katibu wa jumuiya vijana wa umoja wa ccm Mkoa wa Iringa  [UVCCM] James Mgego akisaini kitabu cha wageni


 Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asiah Abdalah akishindwa kujizuwia,akilia kwa uchungu
 Naibu waziri ofisi ya Waziri mkuu anaeshughulikia walemavu Stela Ikupa akilia

Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu akimtuliza Naibu waziri Ofisi ya waziri Mkuu Stela Ikupa























WATANZANIA wametakiwa  kuacha tabia ya kuwaficha watu wenye ulemavu  ndani na badala yake kuwaibua ili waweze kupata haki zao za msingi.
Hayo yamesemwa leo na askofu wa jimbo katoliki la Njombe Alfredy Maluma wakati akitoa homilia yake katika ibada ya  misa takatifu ya mazishi ya kuwaaga na kuwaombea Marehemu mapacha walioungana Maria na Consolata iliyofanyika katika viwanja vya Chuo kikuu cha Katoliki Ruaha Manispaa ya Iringa,Mkoani Iringa.
 Ibada hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali ya seriakali akiwemo waziri wa Elimu Joyce Ndalichako,naibu waziri anayeshugulikiwa walemavu Stela Ikupa,wawakilishi wa wabunge ,wabunge wa mkoa wa Iringa,wakuu wa wilaya wa mkoa wa njombe,viongoze wa  vyama vya siasa,viongozi wa dini.

Akizungumza alisema Taifa linapaswa  kuwapenda na kuwathamani watu wenye ulemavu kama ambavyo shirika la Bikira Maria wa Consolata lilivyojito kuwasaidia walemavu hao katikakipindi chote cha Uhai wao.

Askofu Alfredy alisema kuwa  kumekuwa na wimbi kubwa la wananachi kuwanyanyasa watu wenye ulemavu na wengine kuwaona  mizigo hali inayopelekea watu wenye ulemavu kukosa huduma muhimu wanazostahili kupata.

 Kila binadamu hapa duniani kaumbwa kwa sura na Mfano wa Mungu,hivyo inatupasa tutafakari juu ya wajibu wetu kuhusu  uhai ,tukidhaminiana na na kupendana kwa dhati bila  kubaguana.

 Ibada hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali ya seriakali akiwemo waziri wa Elimu Joyce Ndalichako,naibu waziri anayeshugulikiwa walemavu Stela Ikupa,wawakilishi wa wabunge ,wabunge wa mkoa wa Iringa,wakuu wa wilaya wa mkoa wa njombe,viongoze wa  vyama vya siasa,viongozi wa dini.

Akizungumza alisema Taifa linapaswa  kuwapenda na kuwathamani watu wenye ulemavu kama ambavyo shirika la Bikira Maria wa Consolata lilivyojito kuwasaidia walemavu hao katikakipindi chote cha Uhai wao.

Askofu Alfredy alisema kuwa  kumekuwa na wimbi kubwa la wananachi kuwanyanyasa watu wenye ulemavu na wengine kuwaona  mizigo hali inayopelekea watu wenye ulemavu kukosa huduma muhimu wanazostahili kupata.

 Kila binadamu hapa duniani kaumbwa kwa sura na Mfano wa Mungu,hivyo inatupasa tutafakari juu ya wajibu wetu kuhusu  uhai ,tukidhaminiana na na kupendana kwa dhati bila  kubaguana.


Nae waziri wa elimu,sayansi na teknolijia Profesa Joyce Ndalichako akitoa salamu kwa niaba ya serikali alisema kuwa watanzania wanapaswa kuiga maisha ya Maria na Consolata kutokana na ushujaa wao wa kupambana kuweka bidii katika masomo yao.
Watanzania tunatakiwa tujifunze kupitia maisha ikiwa nipamoja na kujenga utamaduni wa kuvumiliana,kupendana na kushirikiana kuhu tukitafakari kujiepusha mifarakano katika kazi,familia na jamii kwa ujumla.
‘Serikal hii ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk.John Magufuli  inawapenda watanzania wote na imeweka kipumbele kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata Elimu kuanzia msingi mpaka chuo,pia serikali kwa kuwathamini watu wenye ulemavu imeweza kufanya teuzi na tunaona  mawaziri na  mabalozi ambao ni watu wenye ulemavu.

Ndalichako alisema kuwa jamii inatakiwa kuachana na dhana potofu ya kumficha mtoto mwenye ulemavu ndani,na kusema kuwa ulemavu ni maumbile tu  wanapaswa kupata huduma muhimu kama wengine.



0 maoni:

Chapisha Maoni