Jumatatu, 5 Machi 2018

RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA NNE DKT.JAKAYA KIKWETE AUNGA MKONO KWA KUCHANGIA MIFUKO 300 YA SARUJI CHALINZE

Posted by Esta Malibiche  on March 6,2018 IN NEWS

Rais Mstaafu wa awamu ya Nne.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete (Mb)wakishiriki mkutano pamoja na wananchi.

Mbunge wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi CCM,RidhiwaniKikwete,amemshukuru Mbunge wa kwanza wa Jimbo hilo,mabe ni Rais Mstaafu wa awmu ya NNe Dakta Jakaya Mrisho Kikwete kwa mchangomwake wa Mifuko ya saruji 300 aliyoitoa jana kwa ajili ya uendeshaji wa Shughuli za Shule, kukamilisha ujenzi wa kituo cha Afya , nyumba za walimu   Kibindu na Kijiji cha Kwakonje katika kata ya Kibindu. 


Shukrani hizo zimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi CCM,Ridhiwani Kiwete wakati akizungumza na wananchi katika eneo linalojengwa kituo cha Afya na ambapo alishirikiana na wananachi wake  katika ujenzi.
Baad ya kupokea vifaa hivyo,Ridhiwani alimpongeza Rais Mstaafu kwa msaada huo na pia kutambua mchango  mkubwa alioufanya katika jimbo  hilo.

"Tukiwa mkutanoni , tukapata Ujumbe Mzito wa Raisi Mstaafu na Mkulima maarufu akiwa ma Mama Salma (Mb). Ujio wao sio tu ulileta Furaha kwa Wananchi lakini Pia ahadi ya Kuunga mkono juhudi za wanamaendeleo kwa kuchangia Mifuko 300 ya Cementi ilitolewa.Mifuko hii sasa inapelekwa kwa Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji Cha Kwakonje  baada ya kupata Madarasa 8 Msaada toka Tanapa na Milioni 250 toka Serikali Kuu kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Kibindu"" Alisema Ridhiwaninna kuongeza kuwa

Tunamshukuru Mbunge wa kwanza wa Jimbo laChalinze ambae pia ni Rais Mstaafu Dakta Jakaya Mlisho Kikwete,kwa kuchangia Vifaa h(vi.Pia ninawaomba wadau wengine wa Maendeleo kujitoa kwa hali na mali ili kuhakikisha jimbo la Chalinze linasonga Mbele kimaendeleo. 

Kwa upandewake Mh. Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dakta Jakaya  Mrisho Kikwete ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo alisema kuwa lengo la kutoa mifuko hiyo  ni kutokana na kuridhishwa na mwenendo  mzima wa jimbo hilo kwa sasa na kujionea tofauti wake na wa sasa katika upatikanaji wa huduma za wananchi wa chalinze.

Aidha  Dkt Kikwete amempongeza mbunge huyo kwa jitihada anazofanya katika kuhakikisha wananchi wake wanapata maendeleo yenye tija na manufaa  kwa ajili ya kukuza uchumi wao.
"Wakati nikiwa mbunge kulikuwa hakuna mambo mazuri kama yalivyo sasa hivyo  wana chalinze wenzangu nawaombeni tumshike  mkono  mbunge wetu  ili atufikishe salama  kule tuendako alisema.

Aliongeza  kuwa uongozi mzuri ni ule wa kuacha  alama  katika Taifa na hili ndilo naliona mnafanya. 


Kwa Upande wa Mama SalmaKikwete( Mb)  pamoja na kuchangia mifuko ya  Saruji naye pia aliwapongeza hasa wakina mama wa Kibindu kwa jinsi wanavyojitoa kwenye shughuli za maendeleo.








0 maoni:

Chapisha Maoni