Alhamisi, 8 Machi 2018

RC MAKONDA ATANGAZA VITA NA WANAUME WALIOTELEKEZA WATOTO DAR*

Posted by Esta Malibiche ON March 8,2018 IN NEWS

 *Katika Jamii* tunapoona *Mmomonyoka* wa Maadili Hususani kwa *Vijana* kuanza *Matumizi ya Dawa za Kulevya* , Kutukana *Matusi Mitandaoni* tunaanza kulaumu familia, na katika kulaumu *Familia* anaeonekana *Kulaumiwa* Zaidi ni Mama ambae *AMEACHIWA* Jukumu la Kubeba Mimba, kulea na *kutunza Mtoto* Mzigo ambao unakuwa Mzito Kwa Yeye *Kuubeba Mwenyewe* Hatua ambayo Inasababisha *Mwanamke* *kushindwa* Kuhimili na kuanza Kuitwa *Single Mother,* *Single Parents* uku Baadhi ya kina *Baba* wakiingia *Mitini* na kwenda *Kustarehe na Vimada.*

 *RC Makonda* amesema *Tatizo* linakuwa *Kubwa* zaidi pale ambapo *Mama* anaekuja Kubeba *Ujauzito* (mimba) *anapokataliwa* Na *Muhusika* na Kujaribu Kutoa Mimba, mwingine *analazimika* *kutupa kichaga,* au *kufukuzwa* kwao na *Hatimae* anakimbilia Mtaani na Kuanza kuuza *Vitumbua* , *Ndizi* , *Uji* , *karanga,* *samaki* akitafuta hela ya Kutunza Mtoto na kumfanya *Mama Ajute* kwa Jambo Ambalo *walifurahia Pamoja*
, hatua ambayo Imeongeza Maumivu na *Machungu* Mengi kwa *Wanawake* .

 *Mhe. Paul Makonda* amesema Amebaini Idadi kubwa Ya Kina Mama Wanateseka kwa Kukosa Matunzo Stahiki ya Mtoto na Kumpeleka kutoa *Maelekezo* yafuatayo

1. *RC Makonda* Ametoa Muda wa Mwezi Mmoja TU kuanzia Mwezi *March* Mpaka *April* mwaka huu kwa *Wanaume* *WOTE* waliotelekeze *watoto* kwa Wanawake Wanaoishi katika *Mkoa wa Dar es Salaam.* kuwatafuta watoto Wao na kuanza kutoa Matunzo Stahiki

2. *Endapo Agizo la kutoa Matunzo* Stahiki halitafikiwa, *RC Makonda* atakutana na Kina Mama Wote wa *Mkoa wa Dar es Salaam* Wanaoteseka na Kadhia hii kuanzia *Tarehe 09/04/2018* kufika ofisini kwake na Kukutana na Japo La *Wanasheria Nguli* na Maafisa *Maendeleo ya Jamii* ambao watachukua *Hatua* za Kisheria dhidi ya wale wote *watakoshindwa* kutimiza Wajibu wao wa *kisheria* wa *kutunza Watoto.*

3. *RC Makonda* pia ametoa Wiki nzima ya kusikiliza *Malalamiko* yanayohusiana Na *masuala* ya *Malezi* kwa watoto kupata Haki zao *Stahiki* , zoezi ambalo litaanza tarehe *26/04/2018*


*RC Makonda*  amesema Endapo Wahusika Wote Watakaidi Kutekeleza Agizo hilo, Tayari Ameshajiandaa Kuwakabili kwa Kuandaa *jopo la Wanasheria MAHIRI na Maafisa Ustawi wa jamii* watakaoanza kuchukuwa *hatua za kisheria* kwa wanaume wanaokwepa majukumu yao kuanzia *April 09 Mwaka huu* kwenye ofisi ya *Mkuu wa Mkoa* , *Lengo* likiwa ni *kukomesha* Tabia za Unyanyasaji *wanazofanyiwa* Wanawake Pindi wanapoomba au kudai *fedha* za *matunzo* kwa Watoto ambapo Wengi wao huishia *Kupigwa* , *kutukanwa* na *Kunyanyaswa* hatua inayohatarisha *Ustawi* wao na wa *watoto wao.*

 *Mhe Makonda* Amehitimisha kwa kuwatakia *HERI* kina *Mama* Wote katika *Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani* na Kusisitiza *Serikali*ya *Awamu ya Tano* iko pamoja na katika *kuhakikisha* wanatatua *changamoto* kubwa na ndogo zinazowakabili *Wanawake* ili Waweze *Kushiriki* kikamilifu katika Kuijenga *Tanzania Mpya.*

0 maoni:

Chapisha Maoni