Alhamisi, 22 Machi 2018

KATIBU MKUU UWT TAIFA AMINA MAKILAGI AVUNJA NGOME YA CHADEMA IFUNDA,AVUNA WANACHAMA 200

Posted by Esta Malibiche on March 23,2018 in SIASA



Na Esta Malibiche
Iringa
Katibu Mkuu wa  UWT Taifa Amina Makilagi,ambae pia ni mjumbe wa Halmashauri kuu ccm Taifa amevuna wanachama wapya  200 katika kata ya Ifunda Halmashauri ya Iringa vijijini ambao wamejiunga rasmi jana na umoja huo na kupewa kiapo.


Akizungumza na Uwt Kata ya Ifunda Halmashauri ya Iringa Vijijini mara baada ya kuwapokea Wanachama hao,Katibu mkuu  aliwata wanachama wapya kutoa ushirikiano kwa ccm pamoja na Serikali yake ikiwa nipamoja na kuwafichua wale wote wanaokwamisha shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na Serikali  ili  CCM iendelee kushika hatamu.

Makilagi alisema kuwa chama cha Mapinduzi ni chama ambacho kimejengwa kimisingi ya kulea jumuhia  mbalimbali ambazo zipo ndani ya chama hicho ndio maana bado kinanguvu katika siasa za hapa nchini hata kimekuwa mfano kwa nchi nyingine.

Alisema kuwa lengo la ziara hiyo Mkoani Iringa ni kutokana na Agizo la Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Rais John Magufuli kuwataka vipongozi wa chama hicho na Jumuiya  zake, kuacha kufanya kazi kwa mazowea kwa kukaaa ofisini,bali wawatembelee wanachi kujua changamoto zinazowakabili ili ziweze kutatuliwa.


“Jumuiya ya umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi Tanzania ni moja kati ya jumuiya ambayo ipo ndani ya chama hiki na inakazi zake kwa ajili ya kukijenga chama na kuleta maendeleo kwa wananchi waliokipa dhamana ya kuongoza nchi hii” alisema Makilagi


 Aidha Makilagi aliwataka wanawake kujifunza kujitegemea ili waweze kuja kuwaajiri wanaume ambao kwa sasa ndio wamekuwa wakitoa ajira nyingi kwa wanawake hapa nchini.

“Wanawake wenzangu sasa imefika mwisho wa kuwa tegemezi kwa wanaume inatakiwa sasa tusimame sisi kama sisi na tuanze kuwaajiri na kulisha wanaume zenu majumbani kwetu maana tunauwezo wa kufanya kila kazi hizo inatakiwa tujitume” alisema Makilagi

Alisema kuwa wanawake mkiwa mnataka kufanya biashara zenye malengo msiogope kwenda kukopa maana siku hizi kuna mikopo ya bei rahisi na riba yake sio kubwa ambayo itakuwezesha kufanya biashara yako kwa maendeleo yako.

“Ninawaomba msibweteke,huu ni muda wa kuamka  na kuchangamkia fursa zilizopo.Siku hizi Benki nyingi zinawakopesha wanawake na wanawaamini sana wanawake kwenye kufanya biasha hivyo nendeni mkakope msiogope maana hizi benk zipo kwa ajiri ya kusaidia kuinua maisha ya mtanzania” alisema Makilagi

 “Jamani kila pesa ukiitumia kwa nidhamu basi utaona faida yake na itakuletea maendeleo yako na taifa kwa ujumla maana unakuwa umetumia vizuri pesa kwa maendeleo” alisema Makilagi.

















0 maoni:

Chapisha Maoni