Jumatatu, 10 Julai 2017

UVCCM IRINGA YAWATAKA WANAWAKE WAJITOKEZE KWA WINGI KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI

Posted by Esta Malibiche on JULY 10,2017 IN SIASA

Katibu wa umoja wa vijana wa CCM Mkoa wa Iringa (UVCCM) James Mgego (pichani) amewahimiza vijana wa jumuiya hiyo kujitokeza kugombea nafasi za uongozi hasa wasichana  ambao wako nyuma kuchangamkia fursa hizo.

Akizungumza na mtandao huu wa Habari mapema leo hii  alisema kuwa tangu kuanza kwa zoezi hilo ngazi ya mkoa ni vijana 44 tu kati yao wakina dada ni wanne, ikizingatia kuwa mwaka 2017 wa uchaguzi ndani CCM.

Mgego alisema kuwa jumuiya hiyo ni jumuiya ya vijana ya CCM ni kwa ajili ya vijana wote wakiume na wakike lakini inashangaza kuona dada zetu wanakuwa nyuma kuchangamkia fursa za kugombea nafasi za uomgozi ndani ya umoja huo.

Pia katibu huyo aliwataka vijana kuendelea kujitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho na kutowasikiliza watu ambao wapo kuona CCM inakwama katika uchaguzi huo wa ndani ya chama.

Alisema kuwa zoezi la utoaji fomu za uongozi wa UVCCM ngazi ya mkoa ilianza tarehe 02.07.2017 na kukamilika tarehe 10.07.2017 katika ofisi ya UVCCM mkoa wa Iringa na katika ngazi ya wilaya zoezi pia linaendelea na kuongoza kuwa fomu hizo zinatolewa bila malipo.

Mgego alizitaja nafasi hizo za uongozi zinagombewa kuwa ni mwenyekiti UVCCM Mkoa, Mjumbe wa mkutano Mkuu CCM Taifa, Mjumbe Baraza Kuu UVCCM, Mjumbe Mmoja Kuwakilisha UWT, Mjumbe Mmoja kuwakilisha Wazazi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu CCM Mkoa na Mjumbe wa mkutano wa UVCCM Taifa.

“Tulianza na uchaguzi wa mashina umekamilika, ukafuata wa ngazi ya kata naomemalizika na vikao vyake vinaendelea kuchuja wagombea na sasa ni uchaguzi wa UVCCM ngazi mkoa na taifa unaendelea…”alisema katibu huyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni