Jumatatu, 17 Julai 2017

MKUU WA WILAYA YA IRINGA RICHARD KASESELA AWATAKA WAZAZI KUTOWAFICHA WATOTO WENYE ULEMAVU

Posted by Esta Malibiche on JULY 17,2017 IN NEWS

Na Esta Malibiche
Iringa
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka wazazi,walezi na jamii kwa ujumla kuwajali watoto wenye ulemavu kwa kuwapa haki wanazostahili kama watoto wengine.

Kauli hiyo ameitoa mapema leo hii wakati akizungumza na wazazi na watumishi wa kituo cha kulea watoto wenye ulemavu cha Ali Nyumba kilichopo eneo la Wilolesi Manispaa ya Iringa.
Kasesela akiwa kituoni hapo alisema kumekuwa na wimbi kubwa la baadhi ya wazazi na walezi kuwaficha ndani watoto wenye ulemavu  huku wengine wakiwanyanyasa na kutowapa haki stahiki kama watoto wengine  jambo ambalo halistahili katika jamii.
“ Nasikitishwa na baadhi ya wazazi na walezi amabaowanawaficha ndani  watoto wenye ulemavu na wengine wanadiliki kuwatelekeza na kuwatupa bila kujali utu hili halikubaliki.Pia nachukia sana tabia ya baadhi ya akina baba kukimbia watoto wenye ulemavu na kuwachia akina mama kulea peke yao.’’Alisema Kasesela na kuongeza kuwa
Aidha aliwataka maofisa tarafa wafanye utafiti nyumba hadi nyumba kubaini kama kuna mtoto mlemavu,sababu baadhi ya wazazi huwa wanawaficha watoto wao ndani hivyo kuwasababishia kukosa haki zao za msingi.
Awali akisoma taarifa ya kituo hicho mbele ya Mkuu wa Wilaya, mratibu wa kituo hicho Bwana Adam Duma alisema lengo la kuunda umoja huu ulikuwa ni kuwakutanisha wazazi ili waweze kuwa na sauti moja katika kubainisha na kusaidiana katika kutatua changamoto mbalimbali zinazo ikumba jamii ya watoto waishio na ulemavu.
Duma alisema kituo cha Ali Nyumba   kinaendeshwa  kwa msaada wa wahisani mbalimbali ambapo mahitaji makubwa ni pamoja na chakula, baiskeli za walemavu pamoja na gharama za uendeshaji.
‘’Mheshimiwa Mkuu wa Wialaya tumefungua vituo viwili, kimoja kipo hapa wilollesi na kingine Ngome,ambapo Kituo kimoja kinapokea watoto 35.Vituo hivi vinawasaidia watoto wenye ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo kwa kufanya mazoezi ya viungo pamoja na kuwafundisha kazi za mikon’’Alisema Duma.
Katika kituo hiki yupo mtoto aitwaye Zawadi ambaye amesomeshwa hadi kiwango cha darasala saba, Mtoto huyu hawezi kutumia mikono anatumia miguu kwa shida akisaidiwa na kompyuta na amefanikiwa kuandika kitabu kinacho elezea maisha yake’’Alisema Duma.​
Bi.Naumi Patrick ni Mmoja wa wazazi wa watoto wenye ulemavu nae aliwasihii wazazi wenzie kutowaficha ndani watoto wenye ulemavu huku akiitaka serikali iingilie kati kwa mzazi atakaebainika na vitendo vya kikatili na unyanyasali dhidi ya watoto wenye ulemavu
''Kuna baadhi ya wanaume na familia wamekuwa na fikra potofu na kuona kuwa  mtoto mlemavu ni Mkosi katika familia hivyo wanatutelekeza na kutuacha tukilea peke yetu.Sisi tumeona tuungane na kutetea haki ya watoto wetu maana nao wanastahili kupata haki sawa na wengine kama Elimu na Mahitaji muhimu'''Alisema na kuongeza kuwa
''Ninawaomba wazazi wenzangu tusiwafiche watoto wenye ulemavu.Tu jitokeze kupinga huu unyanyasaji dhidi ya vitendo wanavyofanyiwa watoto wenye ulemavu na tuwafichuewale wote wanaowaficha watoto wenye ulemavu ndani''Alisema Bi.Naumi.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  akiwa amemshika Mtoto mchanga ambae ni mlemavu aliyepokelewakwa muda wa wiki moja iliyopita.
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela  akizungumza na Mtoto Zawadi ambae ameandika kitabu  kinachoelezea maisha yake.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akikagua  vifaa vinavyotengenezwa na watoto wenye ulemavu wanaolelewa katika kitu cha Ali Nyumba kilichopo Wilolesi Manispaa ya Iringa
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akikagua  vifaa vinavyotengenezwa na watoto wenye ulemavu wanaolelewa katika kitu cha Ali Nyumba kilichopo Wilolesi Manispaa ya Iringa
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wazazi na watumishi wa kituo cha Ali Nyumba alipowatembelea watoto wenye ulemavu wanaolelewa katika kituo hicho eneo la Wilolesi Manispaa ya Iringa.

0 maoni:

Chapisha Maoni