Jumatatu, 24 Aprili 2017

MWENGE WA UHURU WA WAHAMASISHA MAENDELEO WILAYANI MUFINDI MKOANI IRINGA

Posted by Esta Malibiche On APRIL 24,2017 IN NEWS
 



Na Esta Malibiche
Iringa
Mwenge wa uhuru umezindua miradi 7 ya Maendeleo yenye thamani ya Bill..3,597,714,040.00 katika Halmashauri  ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
Akisoma risala ya utii wa Mwenge wa uhuru 2017 kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli,Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi Riziki Shemdoe alisema kuwa  Miradi iliyozinduliwa,kukaguliwa na kuwekewa jiwe la Msingi  nipamja na barabara iliyopo kata ya Maduma,Mradi wa Maji ,Shamba la mahindi yalitolimwa nawanafunzi wa   shule yaMsingi Maduma  kwa ajili ya chakula cha mchana,ujenzi wa kituo cha Afya Maduma,Club ya kupambana na Rushwa katika shule ya sekondari ya wasichana Mufindi,pamoja na kiwanda cha kuchakata Mbao kilichopo Nyololo.
 ‘’’Mheshimiwa Rais, Wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi,wametekeleza miradi ya Maendeleo ambayo baadhi yake imefunguliwa,kuwekewa jiwe la msingi,kuzinduliwa na kukaguliwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru 2017.Jumla ya miradi 7 imepitiwa na Mwenge wa uhuru,ambapo jumla ya gharama ya miradi yote ni Tsh. 3,597,714,040.00.Alisema Shemdoe
‘’’Mheshimiwa Rais,Halmashauri ya wilaya imechangia tsh.48,000,000,00,Serikali kuu imechangia Tsh.265,884,040.00,Wananchi wamechangia Tsh.103,137,000.00 pamoja na wadau na wahisanimbalimbali Tsh.3,181,00,000.00,vile vile wananchi na wadau mbalimbali wamechangia  fedha taslimu kiasi cha Tsh.18,639,300 ikiwa nipamoja na  vitu halisi na  nguvu zao kwa ajili ya kufanikisha mbio za Mwenge wa uhuru mwa huu 2017.Pia kiasi cha Tsh.5880,800.00 Zimeelekezwa  katika miradi ya maendeleo ya wananchi’’Alisema Shemdoe
Aidha akizungumzia swala la uwezeshwaji kwa vijana wilayani humo  alisema kuwa, jumala ya vijana 4225 wamejiunga na vyama vya kilimo 6 vilivyopo kwenye ngazi ya kata kupitia skimu za Mgololo, Igomaa,Ikweha,Mkonge block Tea Farm,Sawala block Tea na Mtambula AMOCOS.
‘’Mheshimwa Rais,kutokana na Takwimu za sense ya  Taifa ya mwaka 2012,Halmashauri ya Mufindi inakadiliwa kuwa na  jumla ya vijana 148,450[Me 76,298 na Ke 72,152] ambao ni  nguvu kazi ya Taifa sawa na asilimia 53 ya wakazi wote,hadi sasa vijana 2,118 wamenufaika na mikopo yenye thamani ya Tsh. 2,102,469,121 kuroka Tanzania Agricultural Development BANK [TADB] na hali ya marejesho imefikia Tsh. 1,759,832,761  sawa na asilimia 83.70’’’Alisema Shemdoe.
Alisema kuwa ili kuendelea kujenga uwezo wa mfuko wa maendeleo ya vijana,Halmashauri imenga fedha kiasi cha Tsh.169,316,500.00 sawa na asilimia 5 ya mapato ya ndani kwa mwaka huu wa fedha  201|2017 hadi kufikia Aprili 2017 jumla ya Tsh. 150,00,00.00 zimekopeshwa kwa vikundi vya vijana sawa na asilimia 88.6 ya kiasi kilichotengwa,ambapo zaidi ya vijana 1,206 wakiwa katika vikundi wamenufaika.

Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour  akizungumza na wananchi wa wilaya ya Mufindi mara baada ya kupokea  Risala ya utii katika mkesha wa mbio za mwenge uliofanyika kwenye viwanja vya NYololo aliwasihi wananchi kuunga mkono kwa vitendo juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya Tano chini ya uongozi wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kuanya kazi kwa bidii ili Taifa liweze kusonga mbele kiuchumi.
Amour alisema  kuwa serikali imedhamilia kuanzisha viwanda vidogovidogo,vya kati na viwanda vikubwa kwa kutumia rasilimali zinazopatikana hapa nchini,ambavyo vitasaidia kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa, hususani rasilimali zina zopatikana  na kilimo,ufugaji na uvuvi na hatimae kuongeza ajira kwa watanzania.
 ‘’Kauli mbiu ya Mwenge wa uhuru ya mwaka huu 2017 inasema ‘Shiriki kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya ya Nchi Yetu’Hivyo basi Mheshimwa Rais anataka  Taifa liondokane na uvivu ndiyo maana anahamasisha kila mwanmanchi ashiriki katika kukuza chumi wa viwanda kwa kuwataka wawekezaji  kuanzisha viwanda vitakavyotumia  malighafi  zilizopo nchini’’’Alisema Amour.
Aidha aliwasihi wananchi ku dumisha  Umoja ,Amani,Upendo  pamoja na mshikamano kama ulivyoasisiwa na baba wa Taifa na kusema kuwa ili Taifa liweze kusonga mbele kimaendeleo na kupiga hatua kiuchumi Amani inatakiwa kuwepo.








 

0 maoni:

Chapisha Maoni