Jumatatu, 24 Aprili 2017

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MIRADI 7 YENYE THAMANI YA BILL.3 WIAYANI MUFINDI

Posted by Esta Malibiche on APRIL 14,2017 IN NEWS


Kiongozi wa mbio za mbwenge wa Uhuru kitaifa Amour Hamad Amour akizindua mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya  katika kijiji cha Maduma kata ya Mbalamaziwa wilayani Mufindi jana.
Na Esta Malibiche
Iringa
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa  Amour Hamad Amour amewataka viongozi kusimamia kwa ungalifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa iwe na ubora unaotakiwa ,ikamilike kwa wakati na ijengwe kwa kiwango kinachotakiwa kulingana na kiasi  cha fedha kinachotolewa.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akiweka jiwe la msingi katika  mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya katika  kijiji cha Maduma kata ya Mbalamaziwa, unaojengwa kwa nguvu za wananchi kwa kushrikiana na serikali  ambayo mpaka kukamilika kwake utasaidia  kuwahudumia wakazi  zaidi ya 6,158 pia itasaidia kupunguza Msongamano wa wagonjwa katika Hospital ya Wilaya ya Mufindi.
Pamoja na kweka jiwe la msingi katika zahanati hiyo,aligawa vyandarua 80,kwa watoto wadogo na akina mama wajawazioto kujikinga na mbu waenezao malaria
alikagua barabara inayoendelea kutengenezwa, alizindua mradi wa maji safi na salama amoja kukagua shamba la mahindi lenye ulefu hekali  7 lilimwa na wananfunzi wa sshuke ya msingi Maduma kwa ajili ya chakula cha Mchana.
‘’’Ninaziomba shule zote  Nchini kuiga mfano huu,ili wanafunzi waweze kupata chakula cha Mchana wawapo shuleni.Mradi huu ni Mzuri na unahitaji uendelezwe kwa shule zote nchini .Tusiiachie serikali pekee na wazazi wakati wanafunzi wanaweza kutumia muda kidogo kuazalisha chakula’’’Alisema Amour
Aidha kiongozi huyo wa mbio za Mwenge kitaifa aliweka jiwe la Msingi katika kiwanda cha Leshe Investment kinachojishugulisha na kuchakata nguzo za umeme kilichopo Nyololo,alizindua Klabu ya wapinga Rushwa  katika shule ya Sekondari ya Wasichana Mufindi.
Akisoma Taarifa ya Mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya kilichopo kata ya Mbalamaziwa Neema Kyando alisema kuwa, mpaka kukamilika kwa ujenzi huo kutagharimu kiasi cha Tsh.600,000,000.00,ambapo mpaka sasa majengo ya jengo la mapokezi [OPD]umefanyika ,ujenzi wa nyumba za watumishi naendelea kufanyika kwa lengo la watoa huduma katika kituo hichokuwa karibvu na kiutuo cha Afya.
Kyando alisema Lengo la Mradi huo ni kuboresha huduma za Afya katika kata ya Mbalamaziwa ikiwa ipamoja na Afya ya mama na Mtoto.
''Ndugu kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa,Thamani ya Mradi huu mpaka sasa ni Tsh.148,123,500.00,ambapo ujenzi wa mapokezi ya wagonjwa umegharimu kiasi cha Tsh.132,580,000.00 ikiwa mchango wa wananchi ni Tsh.32,947,000.00,Halmashauri ya wilaya Tsh.48,000,000.00,Serikali kuu Tsh.43633,00.00 na wahisaniTsh.8,000,000.00.Ujenzi wa nyumba za watumishi wa Afya umegharimu jumla ya Tsh.15,543,500.00 ikiwa mchango wa wananchi ni Tsh.11,543,500.00 na Serikali kuu Tsh.4,000,000.00 ''Alisema Kyando
Awali mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Willium akipokea Mwenge wa uhuru wilayani humo alisema kuwa ujio wa MWenge wa uhuru wilayani  shughuli za Maendeleo kwa kuwaingia kipato wafanyabiashara katika maeneo ambayo utapita kukagua,kuzindua na kufungua miradi ya Maendeleo.
Jamhuri aliipongeza Serikali ya awamu ya Tano kwa kuunga mkoano juhudi zinazofanywa na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazania Dkt.John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kukusanya mapato kwa kila ngazi na kufanya matumizi yenye tija kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.
‘’’Hii imeuthibitishia umma wa Watanzania kwamba,wewe ni kiongozi Mzalendo mwenye azma ya kweli ya kuwaunganisha Watanzania dhidi ya Mapambano ya Rushwa,mapambano dhidi ya dwa za kulevya,Mapamabano dhidi ya Ukimwi na Malaria.Tunakuhakikishia kwamba tutaendelea kushirikiana na asasi zisizo za kiserikali,viongozi wa dini na wadu wa Maendeleo katika kuhakikisha kuwa,kazi iliyop mbele yetu ni kuhamasisha,kufanyakazi kwa juhudi na maarifa,ili kutimiza mbiu ya Serikali ya awamu ya Tano ya HAPA KAZI TU


 Hata hivyo Taarifa ya ujenzi wa barabara  ya Maduma- Tambalang’ombe Patrick Mwihava alisema Matengenezo ya barabara hiyo ni mkakati wa HALMASHAURI YA WILAYA YA Mfindi,ambayo imejipanga kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bira   za usafiri mna usafirishaji bila matatizo.
Mwihava alisema barabara hiyo imetengenzwa kwa awamu mbili,ambapo awamu ya kwanza  jumla ya kilimota kumi zitafanyiwa matengenezo kwa kiwango cxa changarawe  na mkandarasi aliyepewa tenda ni kampuni ya M/s Willyfres Enterprise Ltd wa Iringa kwa gharama ya Tsh.151,781,040.00 na anatarajia kukamilisha kazi hiyo tarehe 25/5/2017.Pia kwa awamu ya pili itatengenezwa kilomota kumi.
Ndugu kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa,Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hii kutaleta mafanikio makubwa katika kuunganisha maeneo ya kata ya maduma ma Malangali zenye wakazi wapatao 17,828 kwa mujibu wa Sensa ya  wanaokwenda kupata huduma katika kituo cha Afya cha Malangali na kufika katika  Gulio  la Tanmbalang’ombe’’’’Alisema Mwihava.

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour akikagua maradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Maduma



 Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour akizindua maradi wa Maji katika kijiji cha Maduma kata ya Mbalamaziwa
  Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Amour Hamad Amour akimtwisha ndoo ya  Maji Mkazi wa kijiji cha Maduma kata ya Mbalamaziwamara baada ya kuzindua mradi huo


 Jumla ya vyandarua 80 viligawiwa kwa








0 maoni:

Chapisha Maoni