Jumatano, 26 Aprili 2017

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MIRADI 8 YENYE THAMANI YA BILL.2 WILAYANI KILOLO MKOANI IRINGA


Posted by Esta Malibiche on APRIL 26,2017 IN NEWS

Na Esta Malibiche 
Kilolo
HALMASHAURI ya wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa,katika kutekeleza kauli mbiu ya mbio za mwenge wa uhuru kitaifa 2017 inayosema 'Shiriki uchumi wa viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu imeadhimia kuongeza viwanda vidogo vidogo ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kipato cha kati ifikapo 2025.

Akisoma risala ya utii jana kwa Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Katibu tawala wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Yusuph Msawanga alisema kuwa,kutokana na Serikali ya awamu ya tano kudhamiria Tanzania iwe   Nchi ya viwanda  Halmashauri hiyo imetenga maeneo yenye ukubwa wa ekari17,819.91 katika eneo la Lundamatwe,Ilula,Luhanga.Dabaga na Luganga kibaoni kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda.

 Msawanga alisema kuwa kwa sasa  wilaya hiyo inajumla ya viwanda 17 vinavyojihusisha na shuguli mbalimbali zikiwemo usindikaji wa mbao,ukamuaji wa mafuta ya alizeti,usindikaji wa Jam na juisi, pamoja na kiwanda cha  usindikaji  Maji ya kunywa.
‘’’Mh.Rais sisi wananchi wa wilaya ya Kilolo tunakupongeza kwa wewe pamoja na Serikali ya awamu ya Tano kwa kuliongoza Taifa kwa Amani, Upendo, Utulivu na Mshikamano wa Taifa.Pia tunakupongeza  katika kuhakikisha vijana  wanashiriki katika uchumi wa viwanda,kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali,kusimamia utendaji kazi katika utumishi wa umma,kutekeleza mapambano dhidi ya Rushwa,Madawa ya kulevya,Malaria  pamboja na Maambukizi ya vvu\ukimwi’’’’Alisema Msawanga.

Akizungumzia  uimarishaji na uwezeshaji wa vikundi vya vijana na wanawake katika uzalishaji mali alisema wilaya hiyo ina jumla ya vikundi 89, vya vijana vinavyojihusisha na uzalishaji mali vyenye idadi ya wanachama 2,507.Pia vikundi nane vimetoa ajira kwa vijana 73.

Aidha alisema Mwenge wa uhuru mwaka 2017 wilayani kilolo umezidua ,kuweka mawe ya msingi na kukagua miradi  ya Maendeleo katika sekta ya Afya, Elimu,Kilimo,Maji,Maendeleo ya Jamii,Mazingira na Taasisi ya kuzuwia na kupambana na Rushwa Takukuru,jumla ya ikiwa na thamani ya Bill.2,055,857,050.00 ,
Aliongeza kuwa katika utekelezaji wa kauli mbiu za kudumu Mapambano dhidi ya vvu\ukimwi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wilaya  imetekeleza  kwa kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi dhidi ya ukimwi katika kata zote 24 ikiwemo upimaji wa hiari,matumizi sahihi ya kondomu pamoja na kuwahamasisha kutumia dawa za kupunguza makali ya ukimwi na matunzo kwa wanaoishi na vvu.

Mheshimiwa Rais,Mapambano dhidi ya dawa za kulevya kipindi cha kuanzia julai2016 hadi April 2017  wilaya imetekeleza kauli mbiu isemayo ‘Tuwajali na kuwasikiliza  watoto na Vijana’kwa kuendesha misako ya kubaini waingizaji,watumiaji ,wauzaji na wasambazaji wa coceini kwa,Mandrax,Heroine na pombe zilizohifadhiwa kwenye viroba,wamiliki wa mashamba ya bhangi ambapo jumla ya kilogram 23 na gram 60 za bhangi kavu,puli 1 na kete 266 viliakamtwa na kesi zipo mahakamani.’’’Alisema Msawanga.

Kwa upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa,Amour Hamad Amour akizungumza  wanafunzi wa shule ya sekondari Ilula,alisema  kuwa ili Taifa liweze kuwa na viongozi wazuri wenye kuleta Maendeleo lazima wananfunzi ambao ni viongozi wajao wajitume kwa juhudi zote na kufanya bidii  katika masomo yao.

Vitendo vya Rushwa vimeenea katika Taasisi mbalimbali Nchini,tumieni Elimu mnayoipata kukemea vitendo hivyo,muwaheshimu wazazi,Viongozi,walimu,pamoja na kusoma kwa bidii ili kutimiza malengo yenu ya baadae’’’’Alisema Amour.
Nae mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalah akizungumzia Mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria wilayani humo alisema kuwa, ugonjwa wa malaria umekuwa ni miongoni mwa  magonjwa yanayoongoza kwa kuathiri watu wengi wilayani,hivyo kutokana na kauli mbiu yam bio za mwenge wa uhuru 2017 inayosema ‘shiriki kutokomeza Malaria kabisa kwa Manufaa ya Jamii’’aliahidi kuendelea kutoa  Elimu kwa wananchi  juu ya usafi wa Mazingira ili wawezekujikinga na ugonjwa wa Malaria.

Bi.Asia Abdalah aliipongeza Serikali ya awamu ya Tano kwa kuunga mkoano juhudi zinazofanywa na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazania Dkt.John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kukusanya mapato kwa kila ngazi na kufanya matumizi yenye tija kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.

‘’’Hii imeuthibitishia umma wa Watanzania kwamba,wewe ni kiongozi Mzalendo mwenye azma ya kweli ya kuwaunganisha Watanzania dhidi ya Mapambano ya Rushwa,mapambano dhidi ya dwa za kulevya,Mapamabano dhidi ya Ukimwi na Malaria.Tunakuhakikishia kwamba tutaendelea kushirikiana na asasi zisizo za kiserikali,viongozi wa dini na wadu wa Maendeleo katika kuhakikisha kuwa,kazi iliyop mbele yetu ni kuhamasisha,kufanyakazi kwa juhudi na maarifa,ili kutimiza kauli mbiu ya Serikali ya awamu ya Tano ya HAPA KAZI TU.



0 maoni:

Chapisha Maoni