Alhamisi, 20 Aprili 2017

MASHINDANO YA MBIO ZA MAGARI KUFANYIKA MKOANI IRINGA KUANZA APRIL 22-23 MWAKA HUU

Posted by Esta Malibiche on APRIL 20,2017 IN MICHEZO


Mwenyekiti wa kamati ya mbio za magari mkoa wa Iringa Ahmed Mbata kushoto akizungumza na wanahabari leo leo katikati ni mkuu wa habari Iringa Richard kasesela .
 
MASHINDANO ya mbio za magari yanatarajia kufanyika mkoani Iringa kuanzia jumamosi April 22-23 mwaka huu,ambapo madereva 20 wanatarajia kushiriki mashindano hayo yatakayopambwa na ngoma mbalimbali.
Akizungumza na wandishi wa habari jana,Mwenyekiti wa Club za mbio za magari mkoa wa Iringa Hamid Mbata alisema kufanyika kwa mashindano hayo kutaibua fursa nyingi mkoani hapa ikiwa nipamoja na kuongeza kipato katika sekta ya utalii na  wafanyabiashara kutokana na wageni kutoka ndani ya nchi na nje ya nchi watakaoshiriki na kushuhudia mashindano hayo.
"" Kwa siku mbili hizo Mkoa wetu wa Iringautanyenyuka kiuchumi kwa wafanyabiashara na katika sekta ya utalii kutokana na vivutio vingi vizuri vilivyopo lakini havitambuliki kutokana na kutotangazwa,kupitia mashindano haya tutautangaza mkoa wa Iringa na vivutio vilivyopo pia wageni watakaoshiriki na kushuhudia watapata nafasi ya kutembelea vivutio vilivyopo na  hivyo kuliingizia Taifa pato."""Alisema Mbata.
Mbata alisema kuwa umbali wa km 302 zitatumika katika mashindano hayo na washindi watatu watakaopatikana watapewa zawadi ya vikombe kuanzia mshindi wa kwanza hadi wa tatu miaka.
"" Zaidi ya miaka kumi iiliyopita ndipo tulipopata nafasi ya kushiriki madhindano haya ya mbio za magari,ninapenda kuwaahidi wananchibwa mkoa wa Iringa na watanzania kwabujumla kuwa tumejipanga vuzuri kuhakikisha tunafanya vizuri""Alisema Mbata.
Mbata aliwataka wananchi mkoani Iringa na nje ya mkoa kujitokeza kwa wingi kushuhudia mashindano hayo huku wakiwataadhari ya kukaa mbali na barabara zitakazotumika kutokana na mwendo kasi wa mashindano hayo.
Kwa upande wake kaimu mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Iringa Stive Nyandongo aliwataka washiriki kuzingatia swala la usalama barabarani  huku wakizingatia kanuni na kutii sheria zake zilizowekwa.
Nyandongo akisema washiriki wanapaswa kuweka usalama wao kwanza wakati wote watakaokuwa wanaendesha magari hayo na usalama wa raia watakaoshuhudia mashindano hayo ili kujiepusha na madhara yanayoweza kutokea kutokana na kutozingatia swala zima la usalama barabarani.
"Sisi kama polisi tumejipanga vizuri katika kusimamia mashindano haya na kuhakikisha tunaimarisha ulinzi na zoezi hili linamalizika kwa Amani bila kutokea vurugu za aina yeyote.Tunawaomba wananchi ambao wanashi katika barabara zitakazotumika katika mashindano haya wachukue tahadhari wao na mifugo yao sababu magari yatakuwa yanaendeshwa kwa mwendo kasi.Mifugo na watoto wadogo wasiwepo barabarani,waendesha pikipiki(bodaboda)nao wawe makini au wasitumie kwa muda barabara zitakazotumika katika mbio hizo.""" Alisema Nyandongo
Awali mkuu wa wilaya ya Iringa Richard kasesela akizungumzia mashindano hayo aliwataka wananchi kuwa waangalifu kwa maeneo yatakayotumika kutipita mbio hizo.
""" Pamoja na kuyapokea mashindano  kwa mikono miwili lakini yanahatari kubwa kwa watoto waliochini ya miaka 15.Ninawaomba wazazi mhakikishe mnawalinda watoto ili wasipate madhara sababu ya magari ya mashindano hayo kutembea kwa mwendo kasi."""Alisema Kasesela
Kasesela alisema kuwa lengo la mashindano hayo ni kuunyenyua mkoa wa Iringa na kutangaza vivutio vilivyopo ili mashindano ya mbio za magari kwa Afrika na dunia yaje kufanyika mkoani Iringa.
"Ombi kwa wananchi wa mkoa wa Iringa,wajitokeze kwa wingi kushuhudia mashindano hayo huku wakiwa na taadhari ya kukaa mbali na barabara zitakazotumika.""" Alisema Kasesela

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungmza na vyombo vya habari


0 maoni:

Chapisha Maoni