Alhamisi, 20 Aprili 2017

MAKOTA FOREST YAKABIDHI BATI 20 NA MIFUKO YA CEMENT 100 KWA MKUU WA WILAYA KILOLO



 Posted by Esta Malibiche on APRIL 20,17 IN NEWS

Mkuu wa  wilaya ya Kilolo Asia Abdalah (kushoto)  akipokea msaada  wa madawati 20  kutoka kwa  mkurugenzi wa kampuni ya  Makota Forest Bharat Bhesania jana kampuni  hiyo  imetoa madawati  hayo  pamoja na bati 100 kwa  ajili ya  ujenzi wa  vyumba  vya madarasa na  nyumba  za  walimu.

KAMPUNI ya  Makota Forest ya inayojihusisha na  shughuli  za  Kilimo  katika kata ya  Ihimbo  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa imetoa msaada  wa  bati  100 pamoja na madawati  20 kwa ajili ya  kuunga  mkono  serikali ya  wilaya  ya  Kilolo ya ujenzi  wa  vyumba vya madarasa .

Akizungumza leo [jana]   wakati  wa  kukabidhi msaada  huo  kwa  mkuu  wa  wilaya ya  Kilolo Asia Abdalah ,Mkurugenzi  mtendaji  wa kampuni hiyo Bharat Bhesania alisema  kuwa kampuni yake  itaendelea   kusaidia shughuli mbali  mbali za  kimaendeleo katika wilaya ya Kilolo na maeneo  mengine ya  mkoa wa Iringa .

Bhesania alisema kuwa  jitihada  zinazofanywa na viongozi wa  wilaya ya Kilolo na mkoa wa Iringa katika kuwaletea  wananchi maendeleo ni  jitihada  ambazo zinapaswa   kuungwa mkono na  wadau  wote wa maendeleo  ndani ya  mkoa  huo  na  waliopo  nje ya  mkoa .

" Sisi  kama  wawekezaji  tunaowajibu  wa  kuunga  mkono  shughuli  zote za  kimaendeleo  zinazoendelea  katika  maeneo  yetu ....nimekuwa nikisaidia shughuli  nyingi sana na sichoki  kuendelea  kusaidia "Alisema Bhesania

Kwa pande wake Meneja  wa kampuni   Gibson Mkuvalwa  alisema  kampuni  yake  inajihusisha na  kilimo cha mahindi  na  mwaka huu ndipo  shamba  hili  limeanza ila changamoto kubwa  wanayokutana nayo ni  kodi  kubwa  wanayolipa na  kuomba  serikali  kuweza   kuliangalia  hilo.

Mkuvalwa  alisema kupitia kampuni hiyo  wameweza  kutoa  ajira  kwa  wananchi  wanaozunguka kampuni   hiyo  na  wamekuwa  wakijitolea   kutengeneza  barabara  na  kushiriki kwa  nguvu  zote   kuunga mkono shughuli  za  kimaendeleo .

Nae Mkuu wa wilaya ya  Kilolo Asia alisema  kuwa kuwa mwekezaji  huyo ameanza kufungua rasmi  mlango  wa wawekezaji na  wadau  wa maenbdeleo  Kilolo  kuanza  kuchangia  bati na  madawati  na  kuwa  amepata  kufanya  ziara  ndani ya wilaya   hiyo na nje ya  wilaya  kwenda  kuwaomba  wawekezaji na  wadau  wa maendeleo  waliopo  nje ya  Kilolo  kusaidia harambee   hiyo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba  za  walimu .

Alisema  kuwa  msaada  huo wa kampuni ya Makota  Forest  ni  mwanzo wa  wadau  wengine  kujitokeza  kusaidia  harambee   hiyo  na  kuwaomba  wawekezaji  wengine kujitokeza  .

Hezron Nganyagwa ni Diwani  wa kata ya Ihimbowilayani humo nae aliishukuru kampuni hiyo   kwa  msaada  huo  alisema  kuwa utasaidia kwa matumizi  ya  shule  iliyokumbwa na maafa ya  kuezuliwa ambayo wananchi  wameanza  ujenzi  wa  kuta .

0 maoni:

Chapisha Maoni