Jumatano, 2 Mei 2018

Posted by Esta Malibiche on MAY 2,2018 IN KITAIFA



NA ESTA MALIBICHE
KILOLO
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli amemuagiza waziri wa ujenzi, uchukuzi  na mawasilino mhandisi Makame Mbarawa kwa kushirikiana na wakala wa barabara nchini (Tanroad) pamoja na wakala barabara mijini na vijijini (TARURA) kuanza  ujenzi wa barabara ya Iringa-Kilolo kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km.35.
Rais Magufuli amesema hayo jana wakati akiwahutubia wananachi wa wilaya hiyo  Mkoani hapa mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika hospitali ya wilaya ya Kilolo iliyopo mkoani Iringa inayoendelea kujengwa.
“Nafahamu kwamba mnahitaji barabara ya lami na bahati nzuri barabara hii nimenza kujenga kidogokidogo tangu enzi za Venance Mwamoto,serikali hii imetekengeza barabara nyingi sana katika nchi hii na bahati nzuri nimekuwa waziri wa ujenzi miaka 17 lakini kwa heshima ya pekee tutazijenga taratibu.”alisema Dk.Magufulina kuongeza:
“Mna haki ya kuniomba barabara ya lami,Ninachoomba barabara hii ikikamilika muitunze msipakie mizigo mikubwa ili iweze kudumu kwa muda mrefu,inawezekana haikuwapo kwenye bajeti ya mwaka huu lakini jungu kuu haliskosi ukoko.”alisema Dk.magufuli.
Pia Rais Dk. Magufuli ameziagiza halmashauri zote nchini kuanzisha mifuko ya dawa na kuhakikisha fedha zinazoingia kwenye mifuko hiyo zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ikiwamo kununua madawa,vifaa tiba na vitendea kazi vingine.
 Alisema kuwa katika bajeti ya mwaka huu serikali imetenga takribani Bilioni 50 ambazo zitatumika kwa ajili ya kununulia vifaa tiba hospitalini.
Alisema kuwa hospitali hiyo itakuwa na vitendea kazi vyote mara baada ya kukamilika huku akiagiza  wakala wa majengo Tanzania (TBA) kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo haraka iwezekanavyo kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi wa kilolo ili kupunguza vifo vitokanavyo na kina mama na watoto.
Rais Magufuli aliwahakikishia wananchi hao kuwaletea watumishi wa idara ya afya pindi hospitali hiyo ikikamilika atawaletea watumishi wa afya ili waweze kutoa huduma nzuri.
Naye waziri nchi ofisi ya rais tawala mikoa na serikali za mitaa Seleman Jaffo amesema kuwa katika bajeti ya mwaka huu serikali imetenga Bilioni 105 kwa ajili ya kujenga hospitali mpya 67.
Waziri Jaffo alisema kuwa tangu uhuru kulikuwa na vituo vya afya 515, vilivyokuwa na hadhi vilikuwa 115 peke yake lakini kwa sasa serikali inajenga vituo 208 kwa mara moja vinafanyiwa ujenzi mkubwa.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilolo Aloyce kwezi alisema kuwa ujenzi huo utagharimu Sh.Bilioni 4.2 ambayo itajenga majengo saba lakini majengo matano yapo hatua za mwisho lakini majengo ya kuhifadhia maiti na upasuaji yapo hatua za mwanzo.
“Tuliwasilisha andiko kwa katibu mkuu wizara ya fedha lenye thamani ya Bilioni 4.2 lakini hadi sasa serikali imetoa Bilioni 2.28 ambayo ndiyo tuliojenga nayo majengo haya.”alisema Kwezi.
Kwezi aliomba serikali kuwajengea wodi za watoto  na kina mama na waototo ambazo zitagharimu kiasi cha Bilioni 4.6.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema kuwa mkoa wa Iringa ulipokea sh.Bilioni 26 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwamo Elimu,maji,afya,kilimo na barabara.
Awali waziri wa ardhi,nyumba na makazi Wiliam Lukuvi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Isimani mkoani Iringa alionekana kutoridhishwa na baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo kuuza ardhi kinyemela

0 maoni:

Chapisha Maoni