Ijumaa, 25 Mei 2018

JUMLA YA MIRADI 8 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA BILL.6 YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU WILAYANI KILOLO

Posted by Esta Malibiche on Mei 26,2018 IN NEWS

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asiah Abdala.Makabidhiano hayo yamefanyika katika kijiji cha Viwengi ,mpakani mwa Kilolo na Iringa vijijini.PICHA NA ESTA MALIBICHE.

Mkuu wa wilaya ya KiloloAsiah Abdala akipokea Mwenge wa Uhuru mara baada ya kuwasili jana wilayani kilolo.
.Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Charles Kabeho akiweka jiwe la Msingi katika Mradi wa Maji uliopo katika kijiji cha Ilundamatwe kata ya Irole Wilayani kilolo.Mradi huo mapaka kukamilika kwake utagharimu kiasi cha Mill.700.PICHA NA ESTA MALIBICHE.
.Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Charles Kabeho akiweka jiwe la Msingi katika Mradi wa  mtambo wa kutibu nguzo za umeme [New forest ]uliopo kata ya  lundamatwe wilayani Kilolo. 
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Asiah Abdalah,akimsalimia kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Caharles Kabeho.
  Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Asiah Abdalah,akikaribisha wilayani Kilolo  kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Caharles Kabeho
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa Asiah Abdalah,akimkaribisha wilayani Kilolo Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Issa 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Aloyce Kwezi akisamilimana na Kiongozi wa Mio za Mwenge kitaifa Charles Kabeho.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Aloyce  Kwezi akimkaribisha  Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  kitaifa Charles Kabeho

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kilolo akimkaribisha kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Charles Kabeho.
Katibu wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kilolo akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Charlse Kabeho
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Kilolo akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Charlse Kabeho
Mbunge wa Jimbo la Kilolo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM,Venansi Mwamoto akisalimiana na kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa
































































NA ESTA MALIBICHE

KILOLO

MKIMBIZA   Mwenge wa Uhuru kitaifa  Ipyana Alinuswe amewataka wazazi na walezi   Nchini kuhakikisha wanawekeza katika elimu kwa kugharamia mahitaji muhimu ya Watoto wao, kama mavazi, viatu, Madaftari sanjari na kuchangia mchango wa Chakula cha mchana kwa wanafunzi wa kutwa chini ya ujumbe mkuu wa mbio za Mwenge 2018 unaosema “ELimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”
Hayo ameyasema jana wakati akizungumza na wananachi pamoja na wanafunzi katika shule ya Sekondari ya Ilula iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa, wakati akitoa ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 chini ya ujumbe mkuu unaosema “ELimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”
Alinuswe alisema kuwa Serikali ya awamu ya tanao imejipanga kuhakikisha  mitaara ya Elimu inazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuiboresha  mitaara  ili iweze kuzalisha rasilimali watu ambao wataweza kuliletea Taifa Maendeleo.
Akizungumzia utoro mashuleni alisema kuwa swala la utoro kwa wananafunzi linachangiakwa kiasi kikubwa  kuathiri sekata ya Elimu nchini,hivyo ni jukumu la kila mzazi au mlezi kufuatilia maendeleo ya mtoto wake na siyo kuwaachia walimu peke.
Aidha aliwataka wanafunzi kuzingatia masomo ikiwa nipamoja na kusoma kwa bidii huku ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea.
‘Ninawaomba wanafunzi kote nchini msijihusishe na mambo ambayo yanaweza kukatisha ndoto zenu katika masomo.Zingatien masomo mnayofundishwa na walimu wenu,epukeni vishawishi vinavyoweza kuwasababaishia kupata ujauzito’.
Nae kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Charles Kabeho akiwa katika mradi wa nyumba ya walimu uliopo katika kijiji cha Msosa  kata ya Ruaha Mbuyuni,alikataa kuweka jiwe la msingi katika  ujenzi wa nyumba ya walimu iliyojengwa chini ya kiwango ukilinganisha na kiasi cha fedha,ambazo ni Mill.90 zilizotumika kugharimu mradi huo mpaka kukamilika kwake.
‘Kutokana na Mradi huu kukosa sifa kutoana na kujengwa chini ya kiwango,pia kutokana na mradi huu kutoendana na thamani ya fedha,Mwenge wa uhuru hautaweza kuweka jiwe la msingi  katika jingo hili,hakikisheni mnawachukulia hatua ya kinidhamu wale wote waliohusika kukwamisha mradi huu kwa namna moja au nyingine’Alisema Kabeho.
 Aidha Kabeho aliwataka  watendaji kufanya kazi kwa makini huku wakizingatia viwango na ubora katika kutekeleza miradi ya maendeleo ili kuendana na kiasi cha fedha kinachotolewa .

 
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asiah Abdalah akisoma taarifa ya miradi ya maendeleo iliyotembelewa na Mwenge wa uhuru,kabla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Iringa Mjini, alisema alisema  Wilaya yake itaendelea kutekeleza Maagizo mbalimbali yaliyotolewa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kuhusu uboreshaji wa mradi wa nyumba ya walimu iliyopo katika Kijiji cha Ruaha Mbuyuni uliojengwa chini ya kiwango ukilinganisha na fedha zilizotolewa.Pia alimsimamisha kazi mkandarasi aliyejenga chini ya kiwango mradi wa nyumba ya walimu.
‘Kuanzia sasa namsimamisha kazi  mkandarasi na ninaamuru vyombo vya usalama vifanye uchunguzi haraka iwezekananvyo,mpaka kufikia Mei.30 2018 ripoti  ya uchunguzi nipatiwe’Alisema Asiah.
Aidha alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani kilolo ulizindua, kuwekewa mawe ya msingi pamoja na kukaguliwa miradi ya Maendeleo 8 yenye thamani ya shilingi bilioni 6.
Ndugu kiongozi wa Mbio za wa Uhuru kitaifa,Mwenge wa uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo umeweza  kuweka jiwe la msingi katika mradi wa Maji uliopo katika kijiji cha  kitelewasi kata ya Irole, ulizindua mradi wa barabara  ya rami Ilula –Uhambingeto, uliweka jiwe la Msingi katika kiwanda cha kuchakata nguzo za umeme, ,ulizindua maabara za sayansi katika shule ya Sekondari  Kiheka,Ulikagua shuhuli za uzalishaji wa vifaranga vya samaki pia uliweka jiwe la msingi katika mradi wa chumba cha upasuaji katika kituo  cha Afya  mtandika’Alisema Asiah






0 maoni:

Chapisha Maoni