Jumapili, 20 Mei 2018

MAVUNDE AZITAKA HALMASHAURI NCHINI KUTENGA MAENEO KWA AJILI YA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KWA VIJANA

Posted by Esta Malibiche on MEI 21,2018 IN NEWS


NAIBU  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi ,Vijana na Ajira, ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia chama cha Mapinduzi CCM,  Anthony Mavunde amezitaka Halmashauri Nchini kuhakikisha zinatekeleza  agizo la Waziri Mkuu kwa Tawala za mikoa juu ya utengwaji wa maeneo mahususi kwa ajili ya shughuli za kiuchumi za Vijana ili Vijana wengi zaidi wapate fursa za maeneo ya kufanyia shughuli mbalimbali.

Hayo ameyasema jana mara baada ya kutembelea Mashamba  ya Mboga mboga yaliyopo katika  Kijiji cha Kiwele, Halmashauri ya Iringa Vijijini yanayomilikiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa GBRI Co. Ltd Bi. Hadija Jabiri,ambae ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka 27,ikiwa ni moja ya ziara yake ndogo aliyoifanya jana Mkoani Iringa.
Mavunde alimpongeza mjasliamali huyo kutokana na mafanikio makubwa aliyopata kupitia kilimo cha mbogamboga na kuajiri takriban ya wafanyakazi 236 ambao bni vijana  sambamba na uanzishwaji wa mpango wa ushikirishwaji wakulima wadogo wadogo(out-growers) ambao wataiuzuia Kampuni hiyo mazao mbalimbali ya mboga mboga ili aweze kufikia mahitaji ya soko la nje ambalo linahitaji  tani 26  za maharage machanga na njegere change kwa wiki.

‘Ninakila sababau ya kuiomba   Mifuko ya Uwezeshwaji Wananchi Kiuchumi isaidie jitihada hizi zinazofanywa na wajasiliamali walioona wjikite katika kilimo na kujiingizia kipato. Bi Hadija ni kijana mdogo ambae ukulinganisha umri wake ni vitu anavyovifanya hauwezi amini,kaajiri vijana wengi sana ambao pengine wangeweza kuwa wazurulaji lakini wanafanya kazi.Serikali ya awamu ya tano inasisitiza kila mwananchi kufanya kazi,na huu ndiyo utekelezaji wake’Alisema Mavunde









.

0 maoni:

Chapisha Maoni