Jumatatu, 14 Mei 2018

AHMED HUWEL AIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA MBIO ZA MAGARI

Posted by EstaMalibiche on Mei 14,2018 in MICHEZO

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akimkabidhi Kombe la Ushindi Ahmed Huwel aliyeibuka Kidedea katika  Mashindano ya kimataifa ya mbio za magari yaliyohitimishwa jana  mkoani Iringa huku Nchi nne zikishiriki ikiwemo,Tanzani,Kenya,Uganda na Zambia.


NA ESTA MALIBICHE
IRINGA
MSHIRIKI wa mashindano ya Kimataifa ya bio za magari Kutoka Mkoa wa Iringa,Ahmed Huwel ameibuka kidedea kunyakua kombe la mbio hizo huku akiwaacha wenzake 18 kutoka Nchi mbalimbali.
Mashindano hayo yalianza Mei 12,2018  Mkoani Iringa,ambayo yalihitimishwa jana  Mei 13,ambapo nchi nne zilishiriki ikiwemo,Tanzania,Kenya,Uganda na Zambia,huku Mshiriki kutoka Tanzania Mkoani  Iringa,Ahmed Huwel akipeperusha Bendera ya Taifa kwa kuibuka mshindi.
Akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo jana,Mkuu wa Mkoa wa Iringa,Amina Masenza alizitaka Nchi  zilizoshiriki kuendelea kutoa ushirikiano katika Nyanja mbalimbali ili kukuza uchumi wan chi.
‘Mashindano haya yasaidie kujenga urafiki na undugu miongoni mwenu washiriki wa michezo ya ndani na nje ya Tanzania,yasaidie kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika Mkoa wetu wa Iringa,yasaidie kuutangaza utamaduni wa Mkoa wa Iringa ndani na nje ya Tanzani,yasaidie kuimarisha umoja na mshikamano na nchi jirani pia yasaidie kukuza na kuendeleza biashara mbalimbali katika Mkoa wa Iringa n Tanzania kwa ujumla’Alisema Masenza.

Masenza alisema kuwa Uendelezaji wa michezo unahitaji uwekezaji mkubwa hivyo ni jukumu la wadau wote wa maendeleo kuendelea kushikamana ili kuweza kufanikisha kuendeleza michezo katika Mkoa  wa Iringa na Tanzania kwa ujumla.

 ‘Kutokana na umuhimu wa michezo hii na michezo mingine inayochezwa hapa Mkoani Iringa napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba tena wadau mbalimbali wa michezo kuendelea kuchangia shughuli za michezo hapa nchini hususani katika mkoa wangu wa Iringa ambao una vipaji vingi vya michezo’Alisema Masenza.

Akishukuru kwa niaba ya washiriki wa mbio hizo,Ahmed Huwel aliwashukuru washiriki wote kutoka Tanzania na nje ya Nchi kwa kuonyesha ushirikiano toka mashindano haya yalipoanza.
‘Sisi sote ni washindi kwasababau tultoka katika Nchi Zetu tukiwa na lengo moja kwa kila mmoja kuibuka mshindi,lakini tunatakiwa tukubaliane na matokeo yaliyotokea.Huu umoja tulipouonyesha tunatakiwa tuuendeleza katika mashindano yatakayoendelea’Alisema Huwel;
Ninayofuraha kubwa kushinda nyumbani na kuipeperusha bendera ya Taifa.Huu ni ushindi wa watanzania wote na wanairinga kwa ujumla,ninawashukuru sana watanzania kwa kunitia moyo katika safari yangu hii,pale nilipokuwa nimekata tama mlinipa moyo na hatimae leo nimeibuka mshindi’Alisema Huwel.
 

























 





0 maoni:

Chapisha Maoni