Jumatano, 23 Mei 2018

MATUKIO KATIKA PICHA;MWENGE WA UHURU WAANZA ZIARA YAKE MKOANI IRINGA LEO HII

Posted by Esta Malibiche on MEI 23,2018 IN NEWS

  Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza  akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala,makabidhiano hayo yamefanyika leo hii katika kijiji cha Sadani Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.PICHA NA ESTA MALIBICHE

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa akivalishwa skafu na mmoja wa watoto chipukizi ,ishara ya kukaribishwa Mkoani Iringa wakati wakitokea Mkoani Mbeya.


 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza  akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala,makabidhiano hayo yamefanyika leo hii katika kijiji cha Sadani Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi.


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akimkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2018 Charle Francis Kabeho.



Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akimkaribisha mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Charle Francis Kabeho.




Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu akisalimianana Mkimbiza Mwenge kitaifa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2018 Charle Francis Kabeho.

Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asiah Abdalah akisalimianana Mkimbiza Mwenge kitaifa.
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri David Willium akisalimiana na mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela  akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa
 Charle Francis Kabeho.


 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela  akisalimiana na Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa.


 Mkimbiza Mwenge Kitaifa akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina  Masenza



 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa akipokea Mwenge wa Uhuru.

 Mkuu wa wilaya ya KiloloAsiah Abdala akipokea Mwenge wa Uhuru

 Kamanda wa Jeshoi la Zima moto Mkoa wa Iringa akipokea Mwenge wa Uhuru
 




 


















NA ESTA MALIBICHE
IRINGA
MWENGE wa Uhuru 2018 umewasili leo Mkoani Iringa na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza  katika kijiji cha Sadani kilicgopo Haslmashauri ya Wilaya ya Mufindi , ukitokea Mkoani Mbeya,ambapo unatarajia kuzindua,kukagua na kutembelea  miradi  39 ya Maendeleo yenye thamani  ya Bill 24.1
Miradi itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru nipamoja na Elimu, Afya,Maji,Maliasili,Kilimo,Viwanda,Uvuvi   na mradi wa Rushwa.
 ‘Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2018 umebeba kauli mbiu isemayo “Elimu ni ufunguo wa Maisha; Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu.” Kauli mbiu hii inawahamasisha wananchi hususani wa Mkoa wa Iringa  kuwekeza katika elimu kwa kuwapeleka watoto shule ili mkoa wetu na Taifa kwa ujumla upate wataalam wa kutosha ili  taifa letu liweze kupiga hatua kubwa ya maendeleo kwa kuwatumia wataalamu wetu wa ndani’Alisema Masenza na kuongeza kuwa

Pamoja na Kauli Mbiu tajwa hapo juu Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wetu utaendelea kuwahamasisha wananchi kuhusu Mapambano dhidi ya Rushwa,  VVU/UKIMWI,  Matumizi ya Dawa za Kulevya na Mapambano dhidi ya Malaria.
Akizungumzia hali ya maambukizi ya ukimwi alisema kuwa,Mkoa wa Iringa ni wa pili kwa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini kutokana na utafiti wa mwaka 2016\2017 unaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi kimeongezeka na kufikia asilimia 11.3 ikilinganishwa na kiwango cha TAIFA ASILIMI 4.7Kutokana na hali hiyo Mkoa kwa kushirikiana na wadau tunaendelea kutekeleza mkakati wa kupambana na  Ukimwi.

0 maoni:

Chapisha Maoni