Jumanne, 10 Julai 2018

WANANCHI WA MIKUMI WAMSHUKURU RAIS MAGUFULI

Posted by Esta Malibiche on july 10,2018 IN NEWS

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi)Selemani Jafo akiongea viongozi wa wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.
 Waziri wa Nchi, Ofisi Rais, Tawala za Mikoa na Serikali Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa Mikumi juu ya utekelezaji wa ahadi ya Rais Magufuli ya ujenzi wa Kituo cha Afya.
 Ukaguzi wa jengo la zahanati inayotumika kwasasa eneo la Mikumi.

Wananchi wa Mikumi walipokuwa katika mkutano wa hadhara.
..................................
WANANACHI wa Mikumi wamemwagia sifa Rais Dk.John Magufuli kwa kusikia kilio chao cha kukosa huduma za afya.
 Wananchi hao wamemwaga sifa kwa Rais Magufuli wakati Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo alipombelea zahanati ya Mikumi na kuzungumza na wananchi wa mikumi.
 Katika ziara hiyo,Waziri Jafo amewataarifu wananchi hao kwamba serikali inaanza ujenzi wa kituo cha afya Mikumi ambacho kiliahidiwa na Rais Magufuli alipokuwa katika ziara mkoani Morogoro. 
 Kituo hicho kimeshapokea shilingi milioni 400 ambapo ujenzi wa majengo muhimu unatarajiwa kuanza ndani ya wiki moja kuanzia sasa kwa kutumia utaratibu wa force account. 
 Kufuatia habari hiyo, Wananchi wa Mikumi wameishukuru Sana serikali ya awamu ya tano kwamba Rais Magufuli na serikali yake imejipambanua katika kuwahudumia wananchi wanyonge.

Maoni 1 :

  1. Harrah's Casino, Joliet, IL, United States - Mapyro
    Welcome to the casino, 세종특별자치 출장안마 with 고양 출장샵 games and 대전광역 출장안마 poker, 제주도 출장샵 a sportsbook, and 2 bars. 공주 출장샵 The casino has a full selection of slots and poker.

    JibuFuta