Jumatano, 25 Julai 2018

WAZIRI JAFO ATEMBELEA UJENZI WA MIRADI MBALIMBALI WILAYANI BAHI, DODOMA

Posted by Esta Malibiche on Julai 25,2018 IN NEWS

jaf (1)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo akifanya uhakiki wa vipimo vya upana wa Daraja la Chipanga kama vinaendana
na.
jaf (2)
Daraja
la Chipanga lililo katika hatua za mwisho za umaliziaji wilayani Bahi.
jaf (3)
Viongozi
wakikagua maabara iliyoanza kutoa huduma baada ya kumaliza kwa ujenzi katika
kituo cha afya Bahi.
jaf (4)
Zoezi
la ukaguzi wa miradi likiendelea wilayani Bahi.
jaf (5)
Ujenzi
wa daraja la Chipanga lililopo wilayani Bahi Mkoani Dodoma limeleta faraja kwa
wananchi na viongozi wa wilaya hiyo huku wakimwagia sifa Wakala wa Barabara wa Mijini
na Vijijini (TARURA) kwa usimamizi mzuri.
Hali
hiyo imejidhihirisha leo katika ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo alipokuwa akikagua miradi.
Akizungumzia
kufurahishwa na ujenzi huo, Mbunge wa Jimbo la Bahi Omary Baduel amewapongeza TARURA
kwa ujenzi wa daraja hilo kubwa na barabara zake kwa ubora wa hali ya juu
ikilinganishwa na siku za nyuma kabla TARURA haijaanza.
ya maendeleo wilayani Bahi.
Daraja
la Chipanga ni daraja kubwa lenye urefu wa mita 45 na limegharimu Sh. bilioni
2.18 na litakuwa mkombozi kwa wananchi wa Chipanga ambao walikuwa wanateseka
kwa miaka yote.
Katika
ziara hiyo, Waziri Jafo amefanikiwa pia kutembelea ujenzi wa kituo cha Afya
Bahi kinacho karabatiwa na serikali kwa Sh.Milioni 500 ambapo hadi sasa kazi ya
ujenzi imekamilika na wananchi wameanza kupata huduma katika majengo hayo
yaliyojengwa kisasa.

0 maoni:

Chapisha Maoni