Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumatano, 1 Juni 2016

KATIBU MKUU MAMBO YA NDANI ATEMBELEA MRADI WA UZALISHAJI WA NG’OMBE WA MAZIWA GEREZA LA MTEGO WA SIMBA NA GEREZA KUU LA WANAWAKE KINGOLWIRA


kat1Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akipokea salaam kutoka kwa Afisa Mwandamizi wa Jeshi la Magereza, ACP. Shaban Kitolo mara tu baada ya kuwasili katika Gereza Mtego wa Simba katika ziara yake ya kikazi Mei 31, 2016, Mkoani Morogoro(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, CGP, John Casmir Minja.
kat2Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, CGP, John Casmir Minja(kulia) akiongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Projest Rwegasira kuelekea katika Shamba la uzalishaji wa ng’ombe wa maziwa la Gereza Mtego wa Simba.
kat3Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akiangalia kundi la ng’ombe wa maziwa katika shamba la uzalishaji wa ng’ombe wa maziwa Gereza Mtego wa Simba, Mkoani Morogoro. Gereza hilo hivi sasa linafuga ng’ombe wa maziwa 496.
kat4Kundi la ng’ombe wa maziwa wanaofugwa katika shamba la uzalishaji Mifugo Gereza Mtego wa Simba, Kingolwira Mkoani Morogoro wakiwa malishoni kama wanavyoonekana katika picha.
kat5Wafungwa wa Kike katika Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira(walioketi) wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira(meza Kuu) alipofanya ziara ya kikazi gerezani hapo ili kujionea uendeshaji wa Magereza hapa nchini.
kat6Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akionja chakula cha Wafungwa katika Jiko la Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira, Mkoani Morogoro alipofanya ziara ya kikazi ili kujionea Uendeshaji wa Magereza hapa nchini(kulia) ni Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira, ACP. Loyce Ruhembe(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP. John Casmir Minja.
kat7Sajini Taji wa Jeshi la Magereza, Sarah Kabunda ambaye ni Msimamizi Mkuu wa Mradi wa Ufugaji Kuku katika Gereza Kuu la Wanawake Kongolwira akitoa maelezo ya Kitaalam kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira namna Ufugaji kuku unavyofanyika(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).



mbunge  wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu (kulia) akimpokea  waziri wa Kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba alipofanya ziara ya  kikazi wilaya ya Manyoni jana
Waziri Nchemba  akisalimiana na mbunge Nyalandu (kulia)
Waziri  wa  kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  akiwa ameongozana na viongozi mbali mbali  kuingia  ukumbi wa mkutano kati yake na wakulima wa Tumbaku Manyoni
Mbunge Lazaro  Nyalandu kulia akiwa na waziri wa Kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba wakati akisaini kitabu cha  wageni  ofisi ya mkuu wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida
Waziri Nchemba  akiingia ukumbi wa mkutano kati yake na  wakulima wa Tumbaku manyoni
Wakulima wa Tumbaku  wakisalimiana na waziri Nchemba 
Baadhi ya madiwani  wakulima wa Tumbaku manyoni wakimpokea  waziri Mwigulu Nchemba
Baadhi ya  wakulima wa Tumbaku  wakiwa  ukumbi wa mkutano kati yao na waziri Nchemba
Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu  akitambulisha  viongozi mbali mbali kabla ya  mkutano wa  wakulima wa Tumbaku kuanza
Waziri wa  Kilimo , Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  akizungumza na  wakulima wa Tumbaku wilaya ya manyoni mkoa wa Singida jana
Diwani  wa kata ya Mitundu wilaya ya Manyoni Bw Andrea Madole  akimkabidhi nyalaka mbali mbali za uthibitisho wa michango kandamizi  wanayobambikizwa  wakulima wa Tumbaku na Kitengo  cha AMIS   waziri wa  kilimo ,mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ambae alitangaza   kufuta michango  hiyo
Wakulima wa Tumbaku  wakitoa kero  zao kwa  waziri Nchemba (hayupo pichani)
Wabunge  wakisikiliza kero  za  wakulima wa Tumbaku
Waziri wa Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu  wakati  akieleza kilio  cha wakulima wa Tumbaku  wilaya ya Manyoni wakati wa  mkutano wa  waziri Nchemba na wakulima wa Tumbaku  uliofanyika  ukumbi wa CCM Manyoni jana
…………………………………………………………………………………………….
Na MatukiodaimaBlog,Manyoni WAZIRI wa  kilimo ,mifugo na  uvuvi  Bw Mwigulu  Nchemba amefuta michango  hewa iliyokuwa ikichangiwa na wakulima wa Tumbaku  kwa  UNION kwa  kupitia  kitengo  cha AMIS huku akiagiza serikali  ya  wilaya ya Manyoni  kuwachukulia hatua  kali aofisa  ushirika mkoa  Andru Msafiri na afisa  ushirika Wilaya   hiyo Bw Alfred Sekiete iwapo watabainika  kuhusika  deni la bilioni  7  ambalo wanadaiwa benki wakulima  wa tumbaku.
 
Waziri Nchemba  alilazimika kutoa maagizo  hayo  baada  ya  wakulima  wa zao hilo la Tumbaku  kulalamikia utaratibu mbaya wa baadhi ya  viongozi wa UNION na APEX pamoja na baadhi ya maofisa  ushirika   kujinufaisha  kupitia mgongo  wa  wakulima hao.
 
Akitoa agizo  hilo  jana mjini Manyoni  wakati wa  mkutano  wa  pamoja kati yake na  wakulima wa  Tumbaku na viongozi  mbali mbali  wa Serikali  ya  wilaya ya Manyoni na wabunge  wanaotoka  wilaya ya Maeneo  yanayolimwa Tumbaku  mkoani Singida.
 
Waziri Nchemba  alisema  kuwa  baadhi  ya mambo  ambayo serikali  ya Rais Dr John Magufuli  haipendi  kuona ni  pamoja na  wakulima kubebeshwa mizigo mikubwa ambayo kimsingi haiwasaidii kupiga hatua kimaendeleo  zaidi ya  kuwatesa .
 
Alisema  inashangaza  kuona   wakulima  hao  kuendelea  kuumizwa na  viongozi  wachache ambao  wamegeuza  wakulima ni  kichaka cha  wao  kujificha  kujinufaisha  kupitia wakulima.
 
“ Mambo  ya ajabu  sana  hiki kitu  kinaitwa AMIS ni kuwatoza  wakulima michango ya ajabu ajabu  eti  wakulima  kutozwa  dola 1200 kwa  ajili  ya kusafirisha Tumbaku toka  Dar es Salaam kwenda UNION   pia  wanachangia dola 10 kwa  kutunza  kumbukumbu zao  ,dola 3 kupakia na  kushusha mara mchango kwa ajili ya ADMIN   mambo ya ajabu kabisa wakulima wanahusika  vipi na malipo maadmin yani wanatumia lugha  za  kijanja kijanja  kuwaibia  wakulima ADMIN wa makundi kama yale ya Whatsap kwa wakulima  tena…sasa kuanzia leo natangaza  kufuta michango  hii isiyo na maelezo ya kutosha na kuagiza  kujipanga upya kwa  kuwashirikisha   wakulima na taarifa  hiyo ndani ya siku 7 niipate “
 
Waziri chemba  alisema  kuwa kabla ya  kuanza  kuwatoza  wakulima hao michango ni  vizuri  makubaliano ya  michango  hiyo yafanyike  upya kwa kuwashirikisha  wakulima na sio kuendelea  kutumia taratibu  za  zamani ambazo ni mzigo kwa  mkulima.
 
Kuhusu maafisa  ushiriki  kudaiwa  kukopa  benki  kupitia mgongo wa  wakulima  wa  tumbaku na  kupelekea  wakulima hao  kudaiwa  deni  benki  la Tsh bilioni 7 aliagiza mkuu wa  wilaya ya Manyoni kuagiza wakaguzi  na wataalam wake  kufanya  uchunguzi  na iwapo itabainika  kuwa maofisa  hao  walihusika na deni  hilo  hatua  stahiki  kuchukuliwa dhidi 

Heri ya Kuzaliwa Mwanalibeneke wa Lukaza Blog – Josephat Lukaza

Kwanza Napenda kuchukua Nafasi hii Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Kuniwezesha kuiona siku ya Leo maana Si kwa uwezo wangu bali ni kwa Uwezo wake Muumba wetu aliye Juu.

Leo ni siku muhimu sana kwangu maana inanikumbusha siku niliyoletwa Duniani na Mungu kupitia Mama yangu kwa kusudi maalumu hapa duniani.
Napenda Kumshukuru Mungu kwa maana neema na rehema zake ni Za milele. Nasema asante kwa kunifanya kuongeza mwaka mwingine huku nikiwa na afya njema.

Kiukweli Sina cha Kumlipa Mwenyezi Mungu zaidi ya Kumsifu na Kumwabudu yeye kwa maana Sio kwa uwezo wangu.Napenda kuwashukuruni wote Ambao Mmekuwa mkiniombea na kunitakia heri ya kuzaliwa kwangu Nasema asante na Mungu awabariki sana.

Nakukabidhi wewe bwana njia zangu na kukutumainia kwasababu umeagiza kila akukabidhie njia zake na kukutumainia unaenda kumtendea. Zaburi 37: 5 Leo nasema asante sana kwa Maana kila napokuita Wewe unaitika.
Naomba pia uendelee kuziimarisha hatua zangu kwa maana uliagiza katika Zaburi 37:23 Kuwa “Hatua za mtu zaimarishwa na Bwana, Naye aipenda njia yake”
Hakika wewe ni Mungu wa Wote.
Nachukua fursa hii kuwa shukuruni wote Ambao mmenitakia baraka na heri katika siku hii muhimu sana kwangu ambayo inanifanya nitafakari matendo yangu hapa duniani, Uhusiano wangu na Mungu wangu, Uhusiano wangu na Ndugu zangu, Uhusiano na Jamii yangu pamoja na rafiki zangu hakika Namshukuru Mungu sana kwa kuniwezesha kupatana na Ndugu zangu, jamii yangu na hata marafiki zangu. Kiukweli Namshukuru Mungu kwasababu Ni kwa neema zake na Rehema zake ndio zimenifikisha hapa wala sio kwa ujanja wangu wala mimi sio mwema sana kuzidi wengine.
Wewe Ni Mungu wa wote, Huchelewi wala Huwahi Hakika nitakusifu na kukuabudu siku zote za maisha yangu kwa maana matendo yako makuu uliyonitendea Nayaona na kuyafurahia.

Asante sana Mungu wangu naomba uendelee Kutimiza haja za Moyo wangu. Nitaendelea Kukushangilia na Kukusifu kwa maana kila napokuita unaitika.
Happy Birthday to You Josephat Lukaza – Lukaza Blog

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AHUTUBIA MKUTANO WA UMOJA WA MATAIFA WA KUWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI NCHINI PAPUA NEW GUINEI LEO

un1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mzungumzaji Mkuu wa Mkutano wa kuwezesha Wanawake Kiuchumi katika mkutano wa nane kwa Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribean na pacific ACP Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwenye mkutano huo uliofanyika leo Juni 01,2016 katika kituo cha mikutano cha kimataifa PCC Nchini Papua New Guinea.
un2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipongezwa na  Rais Mstaafu wa Nigeria General Olibegan Obasanjo wakati Makamu wa Rais alipomaliza kuhutubia Mkutano wa kuwezesha Wanawake Kiuchumi kwenye mkutano wa nane kwa Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribean na pacific ACP uliofanyika leo Juni 01,2016 katika kituo cha mikutano cha kimataifa PCC Nchini Papua New Guinea. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye Mkutano huo. Katikati Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia Mhe. Natumbo Nandi Ndaitwah.
un3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Rais Mstaafu wa Nigeria General Olibegan Obasanjo wakati Makamu wa Rais alipomaliza kuhutubia Mkutano wa kuwezesha Wanawake Kiuchumi kwenye mkutano wa nane kwa Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribean na pacific ACP uliofanyika leo Juni 01,2016 katika kituo cha mikutano cha kimataifa PCC Nchini Papua New Guinea. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye Mkutano huo. Katikati Naibu waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia Mhe. Natumbo Nandi Ndaitwah.
un4Rais Mstaafu wa Nigeria General Olibegan Obasanjo akimpongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan baada ya  kuhutubia Mkutano wa kuwezesha Wanawake Kiuchumi kwenye mkutano wa nane kwa Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribean na pacific ACP uliofanyika leo Juni 01,2016 katika kituo cha mikutano cha kimataifa PCC Nchini Papua New Guinea. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye mkutano huo.
un5Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mzungumzaji Mkuu wa Mkutano wa kuwezesha Wanawake Kiuchumi katika mkutano wa nane kwa Wakuu wa Nchi za Afrika, Caribean na pacific ACP Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwenye mkutano huo uliofanyika leo Juni 01,2016 katika kituo cha mikutano cha kimataifa PCC Nchini Papua New Guinea. Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye mkutano huo.

DKT SHEIN KUZUNGUMZA NA MABALOZI WILAYA MJINI LEO

zan11Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na wanachama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Kichama,  wakati alipokua akiwapongeza wanachama hao baada ya ushindi wa Uchaguzi marudio uliomalizika mwezi wa Machi mwaka huu,mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani,[Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan12Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na wanachama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Kichama,  wakati alipokua akiwapongeza wanachama hao baada ya ushindi wa Uchaguzi marudio uliomalizika mwezi wa Machi mwaka huu,mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani,[Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan1zan2Wanachama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Kichama,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,wakati alipokua akiwapongeza wanachama hao baada ya ushindi wa Uchaguzi marudio uliomalizika mwezi wa Machi mwaka huu,katika mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani,[Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan3Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Kichana Bi,Fatuma Shomari Juma alipokuwa akisoma risala ya Chama Wilaya ya Mjini Kichama wakati wa mkutano wa kuwashukuru na kuwapongeza wanachama cha Mapinduzi Wilaya hiyo uliofanywa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani, [Picha na Ikulu.] 01/06/2016
zan6Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mjini Kichama Bw. Juma Fakih Choum akiwasalimia wanachama cha mapinduzi waialaya hiyo wakati wa mkutano wa kuwashukuru na kuwapongeza wanachama cha Mapinduzi Wilaya hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein, [Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan7Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mjini Kichama Bw. Juma Fakih Choum  wakati wa mkutano wa kuwashukuru na kuwapongeza wanachama cha Mapinduzi Wilaya hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani, [Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan8Mwanachama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Kichama Bi.Rukia Omar kutoka    jimbo la Kikwajuni alipokuwa akitoa mchango wake wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,alipowapongeza na kuwashukuru Wanachama hao baada ya ushindi wa Uchaguzi marudio uliomalizika mwezi wa Machi mwaka huu,katika mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani,[Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan9Mwanachama cha Mapinduzi wa umoja wa Vijana UVCCM Ashrak Saleh Zingo katika shehia ya kiponda mji Mkongwe wa Zanzibar alipokuwa akitoa mchango wake uliogusia zaidi uvunywaji wa katiba ya Zanzibar unaofanywa na Wanachama cha Upinzania,mchango huo aliuotoa leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani wakati wa Mkutano wa Kuwashukuru Viongozi wa Mashina,wenyeviyi wa Matawi na Maskani uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein, [Picha na Ikulu.] 01/06/2016.
zan10Wanachama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Kichama,wakinyoosha mikono juu kuunga mkono hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein,wakati alipokua akiwashukuru kuwapongeza wanachama hao baada ya ushindi wa Uchaguzi marudio uliomalizika mwezi wa Machi mwaka huu,katika mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa CCM Mkoa Amani,[Picha na Ikulu.] 01/06/2016.

TAARIFA KUTOKA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO (TASWA)

indexA;KAMATI YA TUZO
 
KAMATI ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) imemteua Makamu Mwenyekiti wa TASWA, ambaye pia Mhadhiri Msaidizi wa Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma (SJMC) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Egbert Mkoko kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo za Wanamichezo Bora Tanzania mwaka 2015/2016.
 
Pia TASWA imeteua wajumbe tisa wa kamati hiyo. Majina yao na vyombo vyao katika mabano ni Mahmoud Zubeiry (Bin Zubeiry Sports- Online), Jane John (TBC), Baruani Muhuza (Azam Media), Limonga Justine (Redio Uhuru), Maulid Kitenge (E-FM Redio), Deogratias Rweyunga (Redio One/ITV), Shaffih Dauda (Clouds Media), Asha Muhaji (Bingwa) na Nelly Mtema (Daily News).
 
Kamati inaweza kuongeza wajumbe wengine au kupunguza kwa kadri itakavyoona inafaa. Utaratibu wa kuizindua kamati hiyo unaandaliwa na sekreterieti ya TASWA. Jukumu la kamati itakuwa ni kuandaa utaratibu wa kuwapata wanamichezo watakaowania tuzo hiyo na pia kuteua washindi kwa kila mchezo.
 
Tuzo za Wanamichezo Bora zinazotolewa kila mwaka na TASWA zimepangwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu, Dar es Salaam zikihusisha michezo mbalimbali.
 
B; ZIARA YA MAFUNZO NAIROBI
 
TASWA kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Kenya, vimeanzisha program ya ziara ya mafunzo na kubadilishana uzoefu baina ya vyama hivyo viwili, ikiwa katika makundi tofauti ya wahariri/waandishi waandamizi na kundi lingine la waandishi wa habari chipukizi.
 
Kwa kuanzia wahariri wa habari za michezo 18 au wale wenye uzoefu katika uandishi usiopungua miaka kumi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wataenda Nairobi kwa ziara ya mafunzo kuanzia Julai 6-9 mwaka huu.
Tunaamini wakirudi wataendelea kuwa waalimu wazuri kwa wale chipukizi, ambao nao watapata fursa kama hiyo siku za usoni.
Ahsanteni,
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
01/06/2016

Hifadhi ya Selous yapoteza asilimia 90 ya Tembo wake


imagesNa Daudi Manongi
Hifadhi ya Taifa ya  wanyamapori ya Selous iliyopo kusini mwa Tanzania imepoteza asilimia  90 ya Tembo waliopo katika hifadhi hiyo kutokana na ujangili uliokithiri.
Ripoti ya mfuko wa hifadhi ya wanyapori na mazingira duniani (WWF) imesema kufikia mwaka 2022 kama hakutakuwa na hatua zozote kali zitakazochukuliwa kuwalinda tembo kutokana na ujangili  basi  watatoweka kabisa.
Ripoti hiyo imeendelea kusema kuwa kwa miaka ya nyuma mbuga ya Selous ilikuwa mojawapo ya mbuga kubwa kabisa katika bara la afrika yenye tembo wengi ambapo kulikuwa na tembo zaidi ya 110000 lakini kutokana na ujangili uliokithiri katika miaka 40 iliyopita tembo hao wamepungua na kubakia 15000 tu uku mahitaji makubwa ya pembe za ndovu katika nchi ya china yakitajwa na ripoti hiyo kuwa kichocheo kikubwa cha ujangili na mauaji ya idadi kubwa ya tembo hao.
Aidha ripoti hiyo inaonyesha hathari kubwa  kiuchumi itakayotokea  kutokana na kwamba Tanzania kupitia Mbuga ya Selous inaingiza dola milioni 6 kwa mwaka ikilinganishwa na Sekta ya Viwanda inayochangia dola bilioni 5 katika pato la Taifa.
Pamoja na Hayo Serikali ya awamu ya tano  kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeweka mikakati madhubuti ikiwemo kuunda kitengo chake cha intelijensia na kuunda kanda nane za doria za ushirikiano katika mifumo ya ikolojia ya mbuga ya Selous ambayo imeanza kuwa na mafanikio  ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wadau wa uhifadhi kuwezesha upatikanaji wa vitendea kazi na zana kwa ajili ya doria.
Mwaka 2014 Shirika la Kimataifa la Sayansi,Elimu na Utamaduni la umoja wa mataifa(UNESCO) liliiweka Mbuga ya Selous katika Urithi wa asili ulio hatarini Duniani.