Jumatano, 10 Mei 2017

MWIGULU NCHEMBA MGENI RASMI TAMASHA LA UZINDUZI NYIMBO ZA INJILI MAFINGA

Posted by Esta Malibiche on MEI 10,2017
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba anatarajia kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la uzinduzi wa nyimbo za Injili litakalofanyika siku ya juma pili tarehe MEI 14,2017 kuanzia saa nne asubuhi katika ukumbi wa parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.

 KWAYA KUU YA MTAKATIFU CESILIA PAROKIA YA MAFINGA JIMBO KATOLIKI LA IRINGA,INATARAJIA KUFANYA KUZINDUA  ALBAM YAO YA TATU YA NYIMBO ZA INJILI INAYOKWENDA KWA JINA LA *MBONA WACHELEWA* YESU HUYO.
UZINDUZI HUO UTAFNYIKA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 14/05/2017 KATIKA UKUMBI WA PAROKIA YA MFINGA KUANZIA SAA 10:00 ASUBUHI.
 UZINDUZI HUO UTATANGULIWA NA IBADA YA MISA TAKTIFU,NA MGENI RASMI KATIKA UZINDUZI HUO ANATRAJIA KUWA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI  YA NCHI MH. MWIGULU NCHEMBA (MB),AMBAE ATAAMBATANA NA MBUNGE WA MFINGA MJINI COSATO CHUMI,MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA IRINGA RITHA KABATI NA WAGENI MBALIMBALI WATASHIRIKI UZINDUZI HUO,ZIKIWEMO KWAYA 
MBALIMBALI ZITAKUWEPO KUTOKA MAFINGA NA NJE YA MAFINGA,IkIWEMO 
KWAYA
1. THERESIA WA AVILA -MBEYA
2:KWAYA KUU YA MTAKATIFU CESILIA KIHESA
3: MT. PAUL -DODOMA
4:KWAYA YA MT.CESILIA KILOMBELO
5. THERESIA MTOTO YESU-MAKAMBAKO
6:KWAYA ZA LUTHERANI MAFINGA
7. UINJILISTI ANGLIKANA -MAFINGA
8:UPENDO -KINYANAMBO
9:KWAYA YA BIKIRA MARIA CONSOLATA_MSHINDO IRINGA
10:KWAYA ZOTE ZA RC MAFINGA
11:KWAYA YA MALAIKA GABRIEL MKUU_KILOMBELO
12:KWAYA YA MT.CESILIA IFUNDA.
Na kwaya mbalimbali kutoka Mafinga,na Nje ya Jimbo la Iringa....Hii si ya kukosa.
Nyote mnakaribishwaaa.

Mbunge wa jimbo la Mafinga mjini Cosato Chumi mmoja wa wageni watakaoshuriki Tamasha la uzinduzi wa Nyimbo za Injili kwaya kuu ya Mt.Cesilia Parokia ya Mafinga Jimbo katoliki la Iringa.

Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Iringa Ritha Kabati,mmoja wa wageni watakaoshiri uzinduzi wa Nyimbo za Injili za kwaya ya Mtakatifu Cesilia  parokia ya Mafinga Jimbo Katoliki la Iringa.
Hawa si wengine bali ni wanakwaya wa kwaya kuu ya mtakatofu Cesilia parokia ya Mafinga Jimbo Katoliki la Iringa wanaotarajia kufanya uzinduzi wa Album yao ya Tatu.





Wanakwaya wa kwaya ya Mt.Cesilia kutoka parokia ya Kihesa Jimbo katoliki la Iringa,moja ya kwaya kuu itakayoshiriki Tamasha la uzinduzi wa nyimbo za Injili Mafinga.




 Wanakwaya wa kwaya ya Mt.Cesilia kutoka parokia ya Kihesa Jimbo katoliki la Iringa,moja ya kwaya kuu itakayoshiriki Tamasha la uzinduzi wa nyimbo za Injili Mafinga.



Maoni 1 :

  1. Mhhhhh kwakweli si ya kukosa lazima nije niwashuhudie Cecilia Kihesa watoto wa baba askofu wakifanya yao

    JibuFuta