Kwa Habari za kitaifa na kimataifa

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za michezo na burudani

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za afya

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za Kilimo

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za uchumi na biashara

Tembelea Kali ya habari

Kwa habari za elimu

Tembelea Kali ya habari

Jumatatu, 1 Agosti 2016

Ondoa kitambi kwa kunywa maji mengi kila siku


Katika vitu ambavyo vinawasumbua watu wengi wa maisha ya chini, kati na juu ni kuwa na tumbo kubwa yani kitambi ama kifriza kama wengi wanavyopenda kukiita.
Watu wengi hususani wanaume wamekua wakiongoza kwa kuwa na vitambi ambavyo husababishwa na aina ya vyakula vyenye sukari na mafuta mengi, ambavyo watu wengi huvipendelea kula mara kwa mara, kama ice cream, mikate, keki, chipsi, soseji, nyama, mayai na vyakula vingine vyenye lehemu na carbon kwa wingi.
Madaktari na wanasayansi wa afya ya binadamu wametoa njia mbadala na rahisi ya kupunguza tumbo na kuondoa kitambi ambacho ni mafuta yaliyojijaza kwenye sehemu ya misuli ya tumbo, njia hiyo bora, nyepesi, rahisi na isiyo na gharama ni ya unywaji wa maji kwa wingi kila siku.
Mwanadamu anatakiwa kwa uchache sana anywe lita tano za maji kwa siku, lakini kiwango ambacho ni kizuri na kinachohitajika ni lita saba, maji haya hutumika mwilini katika mifumo tofauti ya ufanyaji kazi wa mwili kama katika kumeng’enya chakula, kuweka ngozi kuwa laini na nyororo, kupunguza uzito na kuondoa mafuta mwilini, lakini pia kupunguza na kuondoa sumu mwilini, Lakini pia maji husaidia kuuweka mwili katika hali ya uchangamfu na wanasaikolojia wamesema maji husaidia kupunguza msongo wa mawazo na humsaidia mtu kutokua na hasira ovyo bila sababu.
Dr.-Oz1
Dr. Mehmet Oz.
Dr. Mehmet Oz kutoka hospitali ya Presbyterian nchini Marekani anafafanua na kukazia zaidi juu ya suala la unywaji wa maji na umuhimu wake kwa binadamu.“mahitaji ya maji yanatofautiana kati ya mtu na mtu. Mambo kama jinsia, hali ya hewa, kiwango cha joto la mwili, ushiriki wa mazoezi, aina ya kazi, umri na aina yam lo unaokula ni mambo yanayotakiwa kuzingatiwa”.
 Imeandaliwa na Hashim Ibrahim
Kitambii

MO Dewji akanusha taarifa ya uongozi wa Simba, tayari ametuma barua kwa uongozi kuomba kuwekeza


Postedy by on Sports

Mohammed Dewji (2)

Siku moja baada ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa Simba na kutolewa taarifa kuwa mwanachama wa klabu hiyo ambaye anatajwa kutaka kuwekeza, Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Makampuni ya Mohammed Enterprises, Mohammed Dewji “MO” amekuwa akizungumza katika vyombo vya habari na hajafikisha maombi yoyote mbele ya uonngozi huo.
Kufuatia taarifaa hiyo ya uongozi, Mohammed Dewji “MO” ametoa ufafanuzi kuhusu jambo hilo na kusema si sahihi kuwa hajawahi kukutana na viongozi wa Simba akiwepo Rais wa klabu, Evans Aveva.
“Nilikuwa nafatilia kwa makini mkutano lakini kulikuwa kunatolewa hoja za upotoshaji kuwa viongozi wanasema nimekuwa ninatangaza tu kwenye vyombo vya habari na wao hawajapokea maombi yoyote kutoka kwangu,
“Nimeshakutana na Rais wa Simba, Evans Aveva zaidi ya mara tatu kujadili hilo jambo, ameshakuja ofisini kwangu na wajumbe wa bodi na Kabour zaidi ya mara tatu, si kweli kuwa nazungumza katika vyombo vya habari hili jambo wanalijua,” alisema MO.
Wakati huohuo, MO amesema tayari ametuma barua kwa uongozi wa Simba kuomba kuwekeza baada ya Rais wa Simba, Evans Aveva kusema kuwa wameridhia kufanya mabadiliko.
Aidha MO amewashukuru wanachama wa Simba kwa kuonyesha kukubaliana na mipango yake ambayo amepanga kuifanyia klabu hiyo pindi atakapopata nafasi ya kununua hisa za asilimia 51 kwa kiasi cha fedha cha Bilioni 20.
“Niwashukuru sana wanachama wa Simba kwa kuwa pamoja na mimi na mimi niwaahidi nitawapigania ili kuisaidia timu yetu na kama tukifankiwatutawapatia hisa bure wanachama ambao wamekuwa wakiipigania Simba,” alisema MO.

MSHAMA: WALIMU WALEVI NA WATORO WASILINDWE/WAFICHULIWE

Mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama,akizungumza na walimu wakuu wa shule za Msingi wilayani humo  ambapo alitoa maagizo mbalimbali ikiwemo kuacha kuwalinda walimu wasio na maadili kazini.Mkuu huyo anaendelea na zoezi la  kukutana na makundi mbalimbali. (Picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha
 
MKUU wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama ,ametoa rai kwa walimu wakuu wa shule za msingi wilayani humo, kuwafichua walimu walevi kazini na watoro pasipo kuwalinda ili kulinda nidhamu kazini.

Amesema wapo baadhi ya walimu wanaoshindwa kufuata maadili yao ya kazi ambapo hakuna hatua zinazochukuliwa.

Aidha Assumpter amewataka walimu hao wakuu kuacha kuwaonea haya walimu hao wanaoshindwa kutimiza wajibu wao wa kazi.

Alitoa rai hiyo ,wakati alipokuwa anazungumza na walimu wakuu wa shule za msingi wilayani hapa ,katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya.

Assumpter aliwaomba wasikubali kukalia tabia hizo ikiwemo kulewa wakati wa kazi kwani kwa walimu wataoshindwa kuwachukulia hatua wanaojihusisha na ulevi,utoro wanaweza kujiweka katika mazingira magumu ya kazi.

Aliwaasa walimu kufanya kazi kwa wito, ari na molari ya kazi ili kuinua kiwango cha taaluma wilayani Kibaha.

"Kufanya vibaya kwa baadhi ya shule ,kunasababishwa na changamoto mbalimbali ikiwemo walimu kujiingiza  na vitendo vya ulevi na utoro,wanakuwa kikwazo katika kuendeleza sekta hii muhimu"

"Walimu wakuu msikubali kuwafumbia macho walimu wa aina hiyo kwani kama mnavyosikia ngazi za juu wanavyowatumbua, huku nako wasipokuwa makini tusiwafumbie macho," alisema Assumpter.

Nae afisa taaluma halmadhauri ya wilaya hiyo, Damas Kimaro alielezea changamoto ambazo zinasababisha kushuka katika ufaulu kitaifa kutoka nafasi ya 4 mpaka ya 9 imechangiwa na mchakato wa uchaguzi mkuu uliomalizika.

Mwalimu Uhai Legeza ,alimtaka mkuu huyo atembelee katika shule mbalimbali ili aweze kujionea namna walimu hao wanavyofanyakazi katika mazingira magumu .

Alisema kuwa baadhi ya walimu hukaa katika ofisi ambazo hazina thamani bora ikiwemo viti na meza wanazotumia hazilingani na nyingi hazina ubora.
"Mkuu tembelea katika shule zetu uone viti na meza tunazotumia katika kutimiza majukumu yetu ya kazi," alisema Legeza.

Kufuatia ombi hilo Assumpter aliahidi kutembelea shule hizo kujionea hali hiyo .
Anasema baada ya serikali kumaliza tatizo la madawati sasa itageukia uboreshaji wa miundombinu ya majengo ili kuhakikisha sekta ya elimu inaboreka zaidi.
Mwisho

Taasisi zatakiwa Kuanzisha Mfumo wa Kupimana

Postedy by Esta Malibiche on August 1.2016 in News No comment

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amezitaka taasisi zilizo chini ya Wizara yake kuanzisha mfumo maalumu wa makubaliano utakaotumika kupima utendaji kazi wa watumishi ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa na kutoa matokeo chanya.

Waziri Mbarawa ameyasema hayo Mkoani Rukwa alipofanya mazungumzo na Viongozi na watendaji wa taasisi hizo wakati alipotembelea mkoa huo kwa lengo la kukagua hali ya miundombinu na kuwaeleza mtazamo mpya wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Amesema katika mfumo huo Waziri ataingia mkataba na wenyeviti wa bodi wakati Katibu Mkuu wa kila sekta kuingia mkataba na watendaji wakuu wa taasisi hizo na watendaji hao wataingia mikataba na wafanyakazi wao ili kuweza kuweka mazingira ya kila mfanyakazi kufikia malengo yaliyowekwa na wizara pamoja na taasisi husika.

“Mimi nitawekeana mkataba na wenyeviti wa bodi za taasisi zote, kwa Sumatra moja ya vipengele vitakavyokuwa kwenye  mkataba huo ni pamoja na mkakati madhubuti wa  kupunguza ajali za barabarani zinazosababisha  vifo kwa Watanzania, TCRA Makusanyo kwenye makampuni ya simu na taaasisi nyingine hivyo hivyo”, amesema Prof. Mbarawa. 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Lt. Mstaafu Chiku Galawa (Kulia) akitoa maelezo ya hali ya miundombinu ya mkoa huo  kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipotembelea ofisini kwake.

Aidha, Waziri Mbarawa amehimiza taasisi hizo kufanya kazi kwa bidii ili kuwajengea miundombinu iliyo bora watanzania ili kuweza kuwafikisha katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Aidha,  Profesa Mbarawa amewataka watendaji hao kufanya kazi kwa ubunifu, kasi na uadilifu ili kuweza  kutatua changamoto zinazowakabili wananchi na kuwajibika kwa ajili ya maslahi ya wananchi na kubadili maisha ya watanzania kwa ujumla.

“Ni wakati wa kutekeleza kauli mbiu ya hapa kazi tu kwa vitendo, hivyo nawataka muwe wabunifu katika utendaji kazi za kila siku na muweze kutoa matokeo chanya ya haraka kwa wananchi”, amesisitiza Prof. Mbarawa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Lt. Mstaafu Chiku Galawa (Kulia) wakati alipotembelea ofisini kwake kupata taarifa ya hali ya miundombinu katika mkoa huo.

Awali akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Lt. Mstaafu Chiku Galawa, Profesa Mbarawa amesema Serikali kupitia wizara yake itaendelea kupandisha hadhi baadhi ya barabara zilizo chini ya Halmashauri na kuwa chini ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), ili kuweza kuendelea kuboresha hali ya miundombinu na kuunganisha mkoa huo na Mikoa ya Mbeya, Rukwa pamoja na nchi zinazozunguka mikoa hiyo kwa barabara za lami.

Profesa Mbarawa amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa huyo kuwa Serikali itaendelea kufanya matengenezo kwa barabara zote nchini kupitia gawio kutoka Mfuko wa Barabara nchini (Road fund) ili kuinua uchumi wa Mkoa.

Waziri Mbarawa yupo katika ziara ya kukagua utendaji kazi kwa wafanyakazi pamoja na hali ya Miundombinu katika mikoa ya nyanda za juu kusini.  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mkoa wa Mbeya Eng. Paul Lyakurwa wakati alipokagua barabara ya Ikana-Makamba –Chitete iliyopo mkoa wa Songwe.
Viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mkoani Rukwa, wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani) wakati alipokutana nao Mkoani Rukwa.

SINAI MISSIONS INTERNATIONAL (SMI) YAFANYA MKUTANO WAKE MKUU WA MWAKA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

????????????????????????????????????Mgeni rasmi kutoka Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Bishop Dr Kameta (katikati) akizungumza na wanachama wa Shirika la kidini linalotoa huduma kwa makanisa na mashirika yanayofanya kazi ya kueneza injili ulimwenguni lijulikanalo kama  SINAI MISSIONS INTERNATIONAL(SMI) wakati wa mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika jijini Dar es Salaam Lengo  la mkutano huo ilikuwa ni kupeana taarifa za utendaji wa SMI na kila huduma chini ya mwavuli wa SMI. kulia  ni Rais wa shirika hilo Ing.Bishop Piter M.Sanga.na kushoto Katibu Mkuu anaemaliza muda wake Bishop Pite W.Chinyama kutoka Zambia.na Mweka Hazina anayemaliza muda wake Msh Raphael Muhagama kutoka Tanzania.
????????????????????????????????????Wajumbe wa Mkutano.
????????????????????????????????????Mkutano ukiendelea.
????????????????????????????????????????????????????????????????????????Wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka wakifuatilia mada mbalimbali.
????????????????????????????????????Viongozi wakimtukuza Mungu kwa wimbo wa pambio wakati wa mkutano mkuu wa mwaka kupeana taarifa za utendaji wa SMI na kila huduma chini ya mwavuli wa SMI.
????????????????????????????????????Wajumbe wa mkutano wakimtukuza Mungu kwa wimbo wa pambio.
????????????????????????????????????Wajumbe wa mkutano mkuu wakimtukuza Mungu kwa wimbo wa pambio wakati wa mkutano mkuu wa mwaka kupeana taarifa za utendaji wa SMI na kila huduma chini ya mwavuli wa SMI.
????????????????????????????????????Mgeni Rasmi kutoka Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Bishop Dr Kameta (kushoto), pamoja na Mtafisiri ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Shirika la MSI, Bishop Gilibert Biyengo.wakihutubia Mkutano Mkuu wa Mwaka.
????????????????????????????????????Mgeni rasmi kutoka Baraza la Makanisa ya Kipentekosite, Bishop Dr Kameta (kushoto) akisaini kitabu cha wageni wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa SINAI MISSIONS INTERNATIONAL(SMI) uliofanyika jijini Dar es Salaam kwaajili ya kupeana taarifa za utendaji wa SMI na kila huduma chini ya mwavuli wa SMI.

JPM AKOSHWA NA DC WA IGUNGA JOHN MWAIPOPO, AAMURU STENDI YA BASI NA SOKO VIANZE KAZI JUMATATU

 Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo akielezea changamoto za Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabiri wilaya hiyo wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016. Mkuu huyo wa wilaya ambaye ana mwezi mmoja toka aanze kazi alimweleza Rais kwamba kuanza kwa stendi ya basi kunasubiri kibali kutoka SUMATRA na kwamba soko jipya ambalo limeshamalizika kujengwa halitumiki kwa sababu ya mkanganyiko unaohusu badhi ya wafanyabishara kuhodhi sehemu kubwa ya soko jipya na kutolitumia huku wakiendelea kufanya bishara kwenye soko la zamani ambako nako pia wana sehemu za Biashara.
  Rais  Dkt Magufuli akiendelea kumsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo wakati akielezea changamoto za Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabili wilaya hiyo wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016
  Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe John Mwaipopo akiandika maagizo ya Rais Dkt. Magufuli kuhusiana na  Stendi ya Mbasi ya abiria na Soko ambapo ameamuru huduma hizo zifunguliwe Jumatatu bila kukosa. Rais ameitaka SUMATRA ihakikishe stendi hiyo inaanza kufanya kazi Jumatatu. Pia ameiagiza halmashauri ya wilaya hiyo kuhakikisha wafanyabishara waliohodhi sehemu za biashara bila kuzitumia katika soko jipya wathibitiwe mara moja.
 Wananchi wa Igunga wanalipuka kwa furaha na Mzee huyu anatoa  noti ya shilingi 10,000/- akitaka kumtuza  Rais Dkt Magufuli kwa kuweza kutatua changamoto za Stendi ya mabasi ya abiria na Soko jipya zinazoikabiri wilaya ya Igunga wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga leo Jumamosi Julai 30, 2016
Rais Dkt Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipokea zawadi ya mchele wa grade One kutoka uongozi wa wilaya ya Igunga  wakati wa mkutano wake wa hadhara mjini Igunga
PICHA NA IKULU

MAADHIMISHO YA KILELE CHA MIAKA 20 YA RADIO MARIA TANZANIA

Postedy by Esta Malibiche On August 1.2016
Mhashamu Baba Askofu Titus Mdoe akiongoza maandamano katika viwanja vya Msimbazi tayari kwa kuanza Ibada ya Misa Takatifu
Antipacy Shinyambala's photo.


DSC_0152
DSC_0156
DSC_0147




DSC_0194
Rais mstaafu wa awamu ta nne Benjamin Mkapa akisalimiana Mgeni rasmi Anna Makinda katika viwanja vya Msimbazi